Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. DKT. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote kwa kuandaa Hotuba na Hoja iliyowekwa mezani.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia eneo moja tu la hali ya usalama wa wananchi katika Mikoa inayopakana na nchi jirani hususan katika Mkoa wa Kigoma. Katika Mkoa wa Kigoma kuna mwingiliano wa wahamiaji/wageni haramu ambao mara kwa mara wanavuka mpaka wa nchi na kuingia nchini wakati mwingine wakiwa na silaha, tena za kivita. Wakati mwingine wahalifu hawa wanaingia nchini kwa kisingizio cha kufanya vibarua mashambani na baadaye wanafanya uhalifu. Uhalifu wa mara kwa mara ni pamoj na kuteka magari, kuua na kuwaibia mali abiria, kuvamia nyumba, kuiba na kubaka wanawake na wasichana na kufanya uhalifu mwingine.

Mheshimiwa Spika, binafsi nimekuwa nafanya mawasiliano ya mara kwa mara na Mheshimiwa Waziri ili kuonesha uzito wa tatizo. Kwa kuwa wahalifu wanavuka mpaka tena wakiwa na silaha, nashauri Wizara yake ishirikiane na Wizara ya Ulinzi na JKT kudhibiti wahalifu kuvuka mpaka wa nchi wakiwa na silaha. Aidha, pale ambapo wahalifu wanafanikiwa kuvuka na kuingia nchini, Wizara yako iangalie uwezekano wa kuanzisha Kanda Maalum ya Kipolisi itakayodhibiti maeneo korofi hususan katika Wilaya za Kakonko, Kibondo, Kasulu na Ngara, katika Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyomweleza Mheshimiwa Waziri tulipokutana katika kikao chake na Waheshimiwa Wabunge wanaotoka Mkoa wa Kigoma, kuna kila dalili kwamba wageni na wahamiaji haramu wanaofanya uhalifu wana ushirikiano mkubwa na wananchi wenyeji wa maeneo husika. Naishauri Wizara itumie ujuzi na pengine kuwaruhusu wananchi kufanya/kupiga kura za siri ili kuwabaini wananchi wanaoshirikiana na wahalifu kutoka nje. Naamini Wizara ina wataalam wa kuendesha zoezi hilo kwa ufanisi bila kuathiri wananchi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.