Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Spika, naungana na wachangiaji waliotangulia kumpongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanazoendelea kuzifanya. Nilipongeze pia Jeshi letu la Polisi kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya ya kutulinda usalama wa raia na mali zetu. Hivi karibuni kumezuka madhehebu mengi sana hususan ya imani ya Kikristo (Pentekoste). Madhehebu hayo mara nyingi hawana ratiba ya kuendesha ibada zao na mara nyingi huendeshwa kwenye makazi ya watu na mara nyingi wanapiga miziki kwa sauti ya juu usiku kucha.

Mheshimiwa Spika, jambo hilo ni kero kwa wakazi wa maeneo mengi. Hivyo naishauri Serikali kuwatengea maeneo maalum madhehebu hayo ya kuendeshea shughuli zao za ibada.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.