Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa hii. Nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa wasilisho zuri na hotuba yenye kuleta matumaini kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Mafia inakabiliwa na ukosefu wa gari la doria baada ya gari lililokuwepo kutumbukia baharini na kuharibika vibaya. Wilaya ya Mafia ni kisiwa kilichopo pembezoni mwa nchi Kusini Mashariki na kinapakana na nchi ya Comoro. Kutokana na ukweli huo, kuna umuhimu mkubwa suala la ulinzi na usalama kuimarishwa sambasamba na kupatiwa boti ya kisasa ya doria ili kuweza kukabiliana na matishio hususani ya ugaidi kutoka nchi za jirani.

Mheshimiwa Spika, makazi kwa Askari Polisi na Magereza, Wilaya ya Mafia ni kero ya muda mrefu sana. Tunaiomba Serikali ijenge nyumba za askari wetu hawa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.