Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo. Makatazo ya vikao vya ndani. Jeshi la Polisi limeendelea kukataza vikao vya ndani vya Vyama vya Upinzani hasa kwa kipindi hiki ambapo wanafanya changuzi za ndani ya chama. Mfano, kikao cha ndani cha wanawake huko Geita tarehe 8 Machi, 2019 Jeshi la Polisi lilizuia kikao cha ndani cha BAWACHA na kulazimisha wanawake hao wa CHADEMA kuungana viwanjani na wanawake wa CCM ambao walikuwa kiwanjani, hii siyo sawa na siyo halali. Naomba Serikali itende haki iache wananchi wafanye vikao vyao vya ndani bila bughudha. Vyama vyote viko kwa mujibu wa Katiba ya nchi, halafu utekelezaji unakuwa kinyume chake.

Mheshimiwa Spika, Polisi wa Barabarani wamekuwa kero kubwa sana kwa wananchi hasa kwa madereva wa hiace na kirikuu. Madereva wanasimamishwa kila kituo ambapo wapo Polisi na wanatozwa fedha. Naiomba Serikali itafute utaratibu wa kudhibiti makosa ya barabarani kwa kutumia mashine badala ya Polisi kuwa barabarani. Wafunge maeneo yote mashine za kubaini makosa mbalimbali na madereva waweze kwenda kulipa faini na kodi zingine kwenye vituo vya polisi bila shuruti.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.