Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa kuipongeza Wizara ya Mambo ya Ndani na majeshi yote. La msingi ni kuhakikisha fedha za maendeleo zinatolewa ili kuwezesha majeshi hayo kumaliza miradi kusudiwa katika maeneo yao.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Katavi unalao tatizo kubwa la makazi ya askari sambamba na makao Makuu ya Mkoa (Jengo la Polisi la Mkoa). Suala hili limepelekea kutumika kwa yaliyo kuwa Makao Makuu ya Polisi Wilaya.

Mheshimiwa Spika, limekuwepo tatizo la msongamano wa wafungwa na mahabusu katika Gereza la Mpanda Mjini. Ombi langu ama ukarabati ufanyike katika gereza hilo au ujenzi wa magereza hasa katika Wilaya Mlele ili kufanya mahabusu toka Mlele wapatiwe huduma huko huko.

Mheshimiwa Spika, suala la mavazi/sare hasa za Askari Magereza na wafungwa naomba litazamwe kwa namna ya pekee maana vazi pia linaakisi kiwango cha utu na ubinadamu ambao ni haki ya msingi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.