Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, nawapongeza wote Waziri na Naibu Waziri pamoja na Katibu Mkuu na wataalam wote ndani ya Wizara kwa kazi nzuri iliyotukuka kwa nchi yetu na wananchi wake. Pia, pongezi za dhati kwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa jinsi anavyoyajali majeshi yetu. Hivyo, nasi wawakilishi tuna kila sababu tukubaliane na tuunge mkono jitihada za Rais kwa kazi kubwa anayofanya kwa majeshi yetu kwani wanafanya kazi katika mazingira magumu hasa makazi, ofisi, sare na miundombinu mingine kutokarabatiwa.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa ushauri kwa Serikali yangu sikivu kuisukuma na kuisisitiza Hazina kutoa fedha zote za maendeleo zinazopitishwa na Bunge kwa bajeti ya Wizara hii kwa Mafungu yote 14, 28, 29, 93 na 51 ili Wizara iweze kutatua changamoto zinazowakabili ambazo ni sugu kwa sasa. Kwa kuwa, hakuna fedha ya maendeleo zilizotoka kwa mwaka 2018/2019 za shilingi bilioni 1.027 na kwa kuwa mwaka haujakamilika ni vema zikatolewa kwa sasa. Mfano Chuo cha Polisi Kidatu kutokana na kutotolewa fedha za maendeleo kimechakaa na kupelekea kupunguza idadi ya wanachuo wanaodahiliwa chuoni hapo na zinahitajika shilingi bilioni 2.6 kwa ajili ya ukarabati.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ni nyeti kiutendaji na tunahitaji wanajeshi wetu kuwa na mpangilio mzuri wa maisha ya kila siku, hivyo maji na umeme ni huduma muhimu kwao. Ni vema tuweke mkakati madhubuti wa kuhakikisha madeni yote ya huduma hizo yanalipwa kikamilifu na yasijirudie.

Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu na kazi ngumu waifanyayo wanajeshi wetu na changamoto lukuki walizonazo ambazo zinawadhoofisha lakini inabidi wafanye kazi ya ziada katika kutekeleza majukumu yao kwa weledi na umakini mkubwa. Wizara inatambua uzito wa changamoto hizo kwa majeshi yetu lakini inapoandaa bajeti wanajielekeza zaidi na ukomo wa bajeti waliopewa na Hazina. Nachokiona ni kwamba ukomo wa bajeti wa sasa haukidhi mahitaji na hawawezi kupata ufumbuzi wa changamoto walizonazo kwa wakati na ukizingatia tabia iliyodumu kwa Hazina kutotoa fedha za maendeleo kwa wakati na zote kama zilivyopitishwa na Bunge.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.