Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kwanza nikupongeze kunipa nafasi ili niweze kuchangia katika hii hotuba ya Waziri wa Mambo ya Ndani. Nampongeza sana kaka yangu Mheshimiwa Lugola, pamoja na Naibu Waziri Masauni pamoja na uongozi wote wa Jeshi la Polisi na Majeshi yote kwa kazi nzuri ambayo mnaendelea kuwatumika watanzania hongereni sana. Yako mambo ambayo ya waziwazi katika hiki kifupi tumeweza kuyaona ambayo watanzania wote naamini watakubaliana na mimi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja suala la ajali kusema kweli Jeshi la Polisi limezisimamia na zimepungua kwa kiasi kikubwa. Lakini kama hiyo haitoshi leo inaweza kufika saa hizi saa mbili nikaondoka hapa kwenda zangu Musoma saa mbili za usiku nikafika Musoma salama pasipokuwa na matatizo yoyote kwa sababu Jeshi la Polisi linafanya kazi nzuri sana. Naendelea kazi yangu ni kuendelea tu kuwaombea kwamba hebu endeleeni kufanya kazi hiyo nzuri watanzania waendelee kuishi kwa amani na utulivu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niombe mambo machache ambayo yamezungumziwa katika hii hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Kati ya matatizo ambayo Serikali na Wizara ya Mambo ya Ndani inapaswa kuyafanyia kazi imesema hapa vizuri kwenye ukurasa wa 11 kwamba Mheshimiwa Rais bilioni kumi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 400 za maaskari wetu na ni ukweli usiopingika kwamba maaskari wetu ni kati ya watu ambao maeneo yao ya kuishi si mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano pale Musoma kwamba ziko nyumba bahati nzuri baada ya kuwa nimepiga kelele toka mwaka 2005 kweli Serikali ikawa sikivu ikaanza kujenga maghorofa mawili pale ambayo yangebeba maaskari wa kutosha. Lakini nakuambia hadi leo tunavyozungumza yale maghorofa yamekamilika kwa asilimia zaidi ya 85 lakini yameshindwa kumaliziwa mara wanaiba milango, mara wanaiba mabomba ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilitaka Mheshimiwa Waziri atuambie ni lini hizi nyumba zitakamilika ili walau wale maaskari wachache waweze kujistili kuliko wanavyoishi sasa wanaishi kwanza wengine uraiani, lakini wengine wanaishi kwenye zile nyumba za full suit ambapo wanaishi kwa tabu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine Mheshimiwa Waziri wewe unafahamu kwamba pale Mjini Musoma pale ndipo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara. Kuna jengo ambalo lilijengwa toka mwaka 2013 jengo la RPC lile jengo limeishiwa kwenye basement hadi leo jengo hilo liko hapo hapo. Sasa nataka nifahamu mpango wa kulijenga jengo hili ili Jeshi la Polisi waweze kufanya kazi zao vizuri. Lakini halikadhalika askari Magereza wote bado hawana nyumba na hata maeneo yao ya kuishi si mazuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni mategemeo yangu kwamba Mheshimiwa Waziri haya majibu utaweza kutufafanulia ili watu wa Musoma waweze kujua namna tunavyoweza kuwasaidia katika haya majengo yaliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko jambo moja kubwa ambalo Mheshimiwa Waziri binafsi nilishalileta kwako, na nilishakuja na Mkurugenzi wa maji, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara pamoja na Magereza Polisi wenyewe wanadaiwa zaidi milioni 850 za maji na Magereza wanadaiwa zaidi milioni 360.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa matokeo yake katika baadhi ya maeneo mengi ya Musoma Mjini kwenye zile Kata za pembezoni kama Rwamlimi, kama Bweli kule Kwanga mpaka kule Makoko tunakosa maji kwa sababu ziko fedha ambazo Jeshi la Magereza pamoja na Polisi walipata huduma lakini ni kwamba wameshindwa kulipa n hizo fedha kama zingepatikana zingetusaidia katika kuboresha maji katika Mji wetu wa Musoma. Sasa ningependa kufahamu mpango wa kulipa haya madeni katika bajeti hii utaweza kutulipa ili walau haya matatizo yaweze kupungua. Pamoja na hayo madeni baada ya kuwa yamelipwa ni imani yangu kwamba yatatusaidia sana katika kuboresha Mji wetu wa Musoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nichangie vilevile kidogo kwenye upande wa Jeshi la Magereza. Nashukuru na tumeangalia pale katika page 28 Mheshimiwa Rais alifanya kazi kubwa ya kuweza kusema kwamba sasa Jeshi la Magereza lazima wajitosheleze kwa chakula na akaonesha kwamba sasa hivi wanalima mnalima kama eka 4,000 na kitu sasa zitalimwa mpaka eka 12,000 na kusema kweli hii ni kazi nzuri ni kazi ya kupongezwa na niseme tu kwamba Jeshi la Magereza wakijipanga vizuri tatizo la chakula hata kwenye Taasisi zetu za Serikali kama shule hilo tatizo litaisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kusema kweli mtu anapofungwa anafungwa mwaka mmoja anafungwa miaka mitatu kulingana na speed ya maendeleo, akitoka kule ndani tunategemea kwamba akienda kule ndani apate nafasi ya kujifunza mambo mengi ambayo ni pamoja na kilimo ni pamoja na ufundi. Sasa tunapowafunga tu na kuwaweka kule ndani akitoka huku nje baadhi ya wafungwa wengi wakiachiwa huru wanatamani warudi ndani ya gereza kwa sababu sasa wanakuta huku nje huku maisha yameenda speed mambo mengi hawayafahamu sasa wanaona kwamba ni afadhali tena arudi magereza kwa sababu kule magereza anapata chakula cha bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naendelea kushauri kwamba mbali na suala la kuwafunza kilimo, vilevile Magereza wanayo nafasi kubwa ya kujifunza mafunzo mbalimbali yanayoweza kuboresha maisha yao. Lakini watakapotoka kule sasa watakuja kwanza wamejirudi lakini watapata mahala pa kuanzia kuliko vile wanavyofungwa, wanakaa mle ndani akitolewa hapo anaenda kusafisha mtalo matokeo yake anatoka kule pasipokuwa na ujuzi. Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba tunapokuwa tunawapeleka mtu anapofanya makosa na akapelekwa Magereza tafsiri yake ni kwamba tunataka ajirudi vilevile ajifunze na baada ya hapo aje kuwa raia mwema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni imani yangu kwamba tukiendelea kuwasaidia hawa Jeshi la Magereza wanaweza wakafanya kazi nzuri zaidi ya kuzalisha na kukuza uchumi wa nchi hii. Baada ya kusema hayo nakushukuru sana kwa kuweza kunipa nafasi. (Makofi)