Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwanza nazungumzia habari ya Jimbo langu la Nkasi Kaskazini, Mheshimiwa Waziri namshukuru sana alifika ziara yake kule akaangalia Gereza la kule kwangu ni la kilimo. Kilimo Kwanza, lakini kilimo hawana dhana za kilimo, wapelekee trekta, Polisi wetu kule mataili ya gari ni shida Polisi Namanyere, petroli, mafuta ya dizeli ni shida ukienda vituo vya pembeni kama vile Kilando na Kabwe ndiyo halikadhalika havifai hata kuviona kwenye macho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Idara ya Uhamiaji Kabwe ukienda kuangalia Idara ya Uhamiaji Mheshimiwa Waziri hali yao ni mbaya, wako mpakani Wakongomani wanaingia kila sehemu kwa gari pale Kabwe lakini hawana chochote cha kuwasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Waziri lazima uwafikirie vya pembeni pembeni, kwanza natoa pongezi sana kwa Polisi tuko hapa Bungeni. Nakaa kule Namanyere mke wangu yuko Namanyere analindwa na Polisi wala sina habari nikimpigia simu asubuhi vipi hali anasema hali salama, wote tuko hapa familia zetu ziko Vijijini kule, wanaotulinda kule ni Polisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nashangaa anakaa Mbunge anasema hapa habari ya Polisi ndugu zangu, hivi Polisi wakigoma masaa matatu tu kila mtu atatoka Bungeni hapa atakimbia mbio hakuna atakayebaki hapa, hakuna atakayebaki Polisi waseme leo tunamgomo kama Madaktari walivyogoma vile Muhimbili hakuna atakayebaki hapa. Lazina tuheshimu Jeshi la Polisi ndugu zangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafanya kazi kulinda mali zetu na sisi wenyewe tumekaa hapa miezi mitatu tukipiga simu majumbani kwetu hali salama kabisa, hakuna hata mmoja ameingiliwa nyumbani kwake kuvunja nyumba, Namanyere sina hata mlinzi nyumbani kwangu yuko mke wangu na watoto lakini yuko salama kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nashangaa unasema habari ya Jeshi la Polisi, ndugu zangu tumefika pabaya ninamheshimu sana Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa uwamuzi aliouchukua kupiga marufuku mikutano. Tukiwa hapa Bungeni wanakwenda kule Majimboni nilizungumza Awamu ya Nne kuanzia asubuhi magazeti, radio, televisheni kutukana, anatoka na mwendawazimu mmoja anajiita Mwenyekiti anaanzisha mkutano kuanzia asubuhi ni kutukana, anamtukana Diwani, anamtukana Mbunge, anamtukana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema kweli kulikuwa hamna nidhamu wote mnakumbuka hapa tulikuwa wakiita mikutano hawa jamaa ilikuwa ni hatari peoples wanaita peoples ni uharibifu wa hali ya juu. Nimeshuhudia kule kwangu hawa jamaa wamechoma nyumba, mpaka akinamama
wamepigwa na mimba zimetoka Kilando kwa ushahidi ninao. Leo mnakuja kusema Polisi, milijifanya Polisi nyie mlishika kwenu Sheria mkononi ilikuwa watu hawatembei ndugu zangu mnatishia namsifu Mheshimiwa Dkt. Magufuli amenyoosha nchi vibaya hii ilikuwa nchi imefikia pabaya. Mlijifanya nyie madume nyie lakini leo wamewashika kusema kweli tunaishi kwa amani na utulivu, tulikuwa sehemu mbaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Kilando kule mpakani tena ndiyo kulikuwa kubaya zaidi mlikuwa mnakuja vifua mbele leo kusema kweli tunashukuru Serikali ya Awamu ya Tano tunatembea na sisi vifua mbele wakati wetu mlikuwa mnadhalilisha wakati wa uchaguzi mdogo tu mnaiba masanduku ya kura, mnachoma masanduku ya kura ushahidi kabisa Jimbo la Kwela kwa Malocha mlichoma masanduku nyie. Kilando wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa Chadema walichoma masanduku ya kura ilikuwa nchi imeharibika sasa imerudi nidhamu, hii ni nidhamu ya hali ya juu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Jeshi la Polisi liendelee na mkazo huo huo, mlikuwa mmetupeleka kubaya mpaka wana CCM wanaogopa kuvaa mpaka nguo za kijani mnawatishia na nyie sasa ni wakati wenu kuacha kuvaa magwanda. Tunakwenda kinidhamu zamu kwa zamu. (Makofi/Kicheko)

MBUNGE FULANI: Keissy sema!

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu lazima tuliona sisi wote nchi ilipofikia tulifikia pabaya nimekaa kule mtu anakuja anaitisha mkutano mnakaa mnamuona kuanzia asubuhi ni matusi tu anamtukana Rais wa nchi. Nilimwambia Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne mimi Mheshimiwa Jakaya Mlisho Kikwete nilimwambia Mheshimiwa takuja kukata mtu kichwa halafu wewe ndiyo utakwenda Mahakamani sitakubali wewe Rais wa nchi unatukanwa nasikiliza na Mapolisi wanasikiliza hawachukue hatua yoyote tulifikia pabaya, hata Polisi walikuwa hawachukue hatua yoyote kwa ushahidi ninao nilizungumza. Wanakumbuka tulikuwa Wabunge Awamu ya Nne hapa nilizungumza, nikamwambia Mheshimiwa Kikwete hawa jamaa wakija kwangu Namanyere wakikutukana tu nitakata kichwa cha mtu, wamezidi hakuna nidhamu dunia nzima hakuna nidhani lazima tuheshimiane. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Mheshimiwa Rais ameweka nidhamu ya hali juu tumuunge mkono na sisi tuendelee tufanye kazi naunga mkono Serikali kusema kweli ndiyo tulisema TV live namna wanazungumzia hovyohovyo live gani hii mazungumzo gani haya wana record kwenye you tube wanasambaza. Lakini hotuba zote mzee ni kichaka ni kuchochea angalieni ndugu zangu, nchi zingine angalieni Libya tangu leo amefariki Gaddafi miaka mingapi Libya imetulia?

MBUNGE FULANI: Haijatulia.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mpaka leo, Libya haijatulia mpaka leo mshukuru ninyi mmekaa hapa familia zenu kule nyumbani mkipiga simu ni salama, ahsante sana. (Makofi)