Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwakunipa nafasi ili nami niweze kuchangia bajeti hii ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Ni ukweli usiopingika kwamba Wizara hii ni nyeti na inafanya kazi kubwa ya kuwahudumia Watanzania takribani milioni 55. Tunashukuru kwa ajili ya usalama na utulivu uliopo ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya watu milioni 55, watu wana tabia na akili tofautilakini ukiangalia jinsi ambavyo Wizara hii kupitia Jeshi lake la Polisi imeweza kudhibiti hali ya uhalifu ndani ya nchi hii, tuna kila sababu ya kuwapongeza. Kwa hiyo, nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri mwenye dhamana, Naibu Waziri, Makamishna Jenerali wa Uhamiaji, Jeshi la Magereza na Jeshi la Zima Moto na Uokoaji kwa kazi kubwa ambayo kwa kweli wameweza kuifanya, tunawapongeza na Mungu awabariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Wakati wote hauwezi ukafanya kwa asilimia 100, we always do to optimum. Kwa hiyo, kwa jitihada ambazo zimefanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika kuhakikisha kwamba utulivu na amani unapatikana kupitia Wizara hii ya Mambo ya Ndani, tuna kila sababu ya kusema wamefanya kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kwamba changamoto hazikosi, kwenye Jeshi la Polisi kama wengine ambavyo wamesemakwamba zipo changamoto hususan katika uwezeshaji wa Jeshi letu la Polisi kutekeleza majukumu yao kulingana na hali ya kijiografia ya nchi yetu na ukubwa wa nchi yetu. Tunajua kwamba resources, kwa maana ya rasilimali ni kidogo, hasa rasilimali watu lakini pia hata vitendea kazi. Tunamshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi ambavyo anaendelea kuguswa kwa namna ya kipekee ili kuiwezesha Wizara hii kutekeleza majukumu yake.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo changamoto ya malazi, kwa maana ya nyumba za Askari wetu, ipo changamoto hata ya matumizi ya kila siku kwa maana yabills za umeme, na maji. Niombe Wizara ijaribu kuangalia maeneo ambayo kwa kweli kuna madeni makubwa kama ambavyo Kamati imeweza kushauri, basi waangalie ni namna gani wanaweza kupunguza madeni hayo kwenye maeneo ambayo madeni ya umeme na maji yapo ikiwa ni pamoja na Wilaya yangu ya Ngara. (Makofi)

MheshimiwaMwenyekiti,lakini pia tunajua kwamba jiografia zinatofautiana, kwamfano, Wilaya ya Ngara iko mpakani, tunapakana na nchi mbili ambazo hali ya usalama wakati mwingine inakuwa si tulivu na katika mipaka yetu kunakuwa na changamoto ya mwingiliano na wageni kutoka nje. Hii inatokana na kwamba Wilaya ya Ngara kwa muda mrefu ime-host wakimbizi, tangu miaka ya 1959. Kwa hiyo, Wilaya ya Ngara ni Wilaya ambayo sasa hata wageni kutoka nchi jirani wameshaizoea kutokana na kwamba wameishi kwa muda mrefu wakiwa wakimbizi, kwa hiyo, hata wanapokwenda ni rahisi kurudi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tuombe vituo vya polisi ambavyo sasakwa jitihada za wananchi kwa kushirikiana na viongozi wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Mkoa, tumeanza kujenga kwenye maeneo hasa kata za mpakani, basi Wizara ione namna gani inavyoweza kutuongezea nguvu kwa ajili ya kukamilisha vituo hivyo. Vituo hivyo ni Mkanizi, Mluvyagira, Murubanga, Keza na maeneo mengine.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,Wilaya ya Ngara ina vituo viwili vya pamoja, OSBP (One Stop Border Posts) kwenye mpaka Rusumo tunapopakana na Rwanda na mpaka wa Kabanga tunapopakana na Burundi. Kituo hiki cha OSBP- Rusumo, tunahitaji kuwa naCCTV Cameras, hakuna, ukienda upande wa Rwanda kila ofisi ina CCTV Camera, kwetu pale hakuna hata moja, kwa hiyo, kiusalama ni changamoto kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,lakini pia tumepita pale na Kamati ya LAAC kuangalia kituo hiki, tunazo scanners mbili, scanner kwa ajili ya passengers na kwa ajili ya luggage’s. Scanners zile zinahitaji moto mwingi wa umeme, wakati mwingine hazifanyi kazi, kwa hiyo, upekuzi unafanyika manuallykiasi kwamba kiusalama si hali nzuri, tunahitaji kuboresha maeneo yale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda upande waJeshi la Magereza, tuna changamoto kubwa hasa Wilaya yangu ya Ngara, kwanza hawana gari, hata wanapokuwa na wagonjwa kuwasafirisha kuwapeleka hospitali ni tatizo lakini hata kuwapeleka wafungwa kwenye shughuli inakuwa ni gumu, hasa inapokuwa maeneo ya mbali. Kwa hiyo, tunahitaji tupate garikwa ajili ya Jeshi letu la Magereza katika Wilaya yetu ya Ngara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni pamoja pia na msongamano wa wafungwa/mahabusu magerezani. Wapo mahabusu ambao hawana sababu ya kuendelea kukaa mle kwamuda mrefu kutokana na kesi zao walizo nazo. Wengine kesi zao zina dhamana, kwa hiyo, tukiweza kuharakisha kufanya upelelezi au wakapewa dhamana wakawa nje wakawa wanahudhuria mahakamani, inaweza ikapunguza msongaman. Kwa hiyo, niombe hilo nalo liweze kufuatiliwa na kuangaliwa kwa umakini hii ikiwa ni pamoja na wahamiaji haramu ambao anakamatwa na kuwekwa ndani kwa muda mrefu. Kama inabainika kwamba ni wahamiaji harama hakuna sababu ya kuwahifadhi na kuwagharamia chakula na kadhalika, ni afadhali tukawarudisha kwa sababu wengi wanatokea nchi za jirani, Rwanda na Burundi, ambayo ni just walking distance, kutoka Ngara Mjini kwenda borders hizo zote, hazizidi kilomita 30. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,nikienda upande wa Uhamiaji, tunatambua kwamba Sheria ya Uraia wa Tanzania ya mwaka 1995, Sura ya 357 na kama ilivyorejewa mwaka 2002 lakini na Kanuni zake za mwaka 1997, zinaeleza kwamba raia wa Tanzania wanatambuliwa kwa aina tatu: Uraia wa Kuzaliwa;Uaraia wa Kurithi lakini na Uraia pia wa Kuandikishwa. Utambuzi huu unazingatia vipindi mbalimbali vya uongoziwa nchi hii. Kuna uraia kabla nabaada ya uhuru,kabla ya mapinduzi na baada ya mapinduzi na baada ya Muungano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba wanasema ignorance of the law is not excuse lakini tunahitaji kuendelea kutoa elimukwa wananchi wetu na wakati mwingine kuweza kuhakikisha kwamba haya makundi matatu ya uraia yanajulikana katika jamii. Wakati mwingine hata zinapotolewa taarifa kwamba kuna baadhi ya wahamiaji haramu, unajikuta watu wengine wanapata usumbufu kumbe wako katika categorieshizi na hawapaswi kutuhumiwa kama siyo raia lakini ni kutokana nakwamba elimu hii ya uraia kwa wananchiwalio wengi hususan maeneo ya vijijini na hasa maeneo ya mipakani haipo. Kwa hiyo, tuombe Jeshi letu la Uhamiaji wajaribu kujisumbua hasa katika maeneo ya mipakani na vijijinikutoa elimu ya uraia ili kuweza kujua nani anakuwa raia na nani si raia na kwa sababu zipi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru Mheshimiwa Waziri mwanzoni mwaka huu ulifanya ziara katika Wilaya yangu ya Ngara, tumekuwa waathirika wakubwa hususan katika suala zima la uraia. Kuna wapiga kura wangu wengine wanashindwa hata kutembea kwenda Kahama lakini kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Sura ile ya Kwanza, Uhuru wa Kuishi, Mtanzania anayo haki ya kuishi mahali popote. Wakati mwingine wananchi wanashindwa kutembea kwa kuhofu kwambaakionekana sehemu fulani …

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Gashaza, ahsante sana. (Makofi)

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.