Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nitazungumzia mambo matatu kwanza kuhusiana na mikutano ya kisiasa, pili kuhusiana na Mashekhe ambao wapo jela sasa, ramadhani sita wapo jela, kisha nitazungumzia juu ya ajira ya askari wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote humu tumeapa kuheshimu katiba pamoja na viongozi ambao hawapo humu ndani, na katiba yetu maeneo mengi inaeleza juu ya haki, usawa, uwadilifu, ya namna ya ku- treat haki za watu na mambo mengine. Lakini pia inatupa fursa ya namna ya kujikusanya kujieleza, kujiunga, uhuru huo umetolewa, lakini pia nchi yetu imejiunga na mikataba mbalimbali imesaini mikataba mbalimbali ya kimataifa juu ya haki ya kujikusanya na kujieleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mwaka 92 kwa hiari yetu tulikubali kwamba tunaingia katika mfumo wa vyama vingi, na CCM kwa nafasi yake iliyokuwa ilikuwa inaweza kukataa kutokuingia katika vyama vingi. Kwa sababu kwanza wale walisema wanataka vyama vingi walikuwa ni kidogo 20 percent lakini ikaonekana busara kwamba 20 percent hawa wanaweza wakawa wamenyimwa haki yao kwahivyo tuwape haki na tukakubaliana tuingie kwenye mfumo wa vyama vingi. Lakini seven year on haionekani infact it is even going to the extreme. Kwamba CCM sasa wanakataa kilekile ambacho wao walituingiza ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa unashangaa nchi hii kwamba inaamini katika demokrasia, inaamini katika siasa za pluralism kwa sababu haielekei kwamba inaamini hivyo kwa matendo, ndani ya katiba ndani ya sheria tunasema kama tunafuata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema tutazungumza habari ya mikutano ni simple logic it doesn’t need Ph.D au rocket science, kwamba ili mtu afanye siasa lazima aweze kuchanganyika na watu, ili mtu afanye siasa lazima aweze kujikusanya na watu, aweze kuzungumza na watu, aweze kupiga propaganda na sera zake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tumesema mara nyingi kama mnahisi hamuwezi bado mna-majorit just call it off semeni tu mnazo kura za kutosha humu za kusema kuanzia leo hakuna vyama vingi basi tujuwe hakuna vyama vingi tusisumbuane tusitaabishane tusipatishane tabu, kwamba mnataka vyama vingi inaelekeaje mnataka vyama vingi mtu mmoja anasema siasa msimu mpaka msimu mnataka vyama vingi lakini bado hamruhusu watu wafanye mikutano, mnataka vyama vingi lakini bado mnakuja na excuse lame excuses intelligentsia sijui kitu gani kitu gani jamani kama intelligentsia umeipata si ndiyo wewe wakuifanyia kazi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa you’re a failure ukiwa na intelligency you’re a failure sasa kama Waziri unakubali uitwe failure is horrible kama unakubali uitwe failure kila siku unakubali polisi wako wakuwa intelligentsia you don’t question kama intelligentsia kwanini usiwape wape opition. Juzi ulisema hapa katika kujibu swali moja ulisema kwamba kama mkutano leo haufanyiki unakuwa kesho kutwa ufanye nafikiri ilikuwa katika briefing hebu nikuulize, siku gani upinzani walipewa siku mbadala ya kufanya mkutano? Hata siku moja! (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, sitaki kuzungumza habari ya CCM wala nazungumzia kuwakilisha wapinzani kwahiyo kama mnahisi hamuwezi call it off. Leo leteni Muswada na sisi tutaunga mkono tutafanya kazi nyingine siyo lazima kuwa wapinzani si lazima kuwemo humu ndani hatukuzaliwa kuwa Wabunge wa upinzani tumezaliwa tuishi tu kuwemo humu ni coincidence tu, kwa hiyo, siyo lazima tubakie humu kama hamtaki wacheni semeni hakuna vyama vingi katika nchi hii mtakutana nao mabwana wa dunia (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kuhusu mashekhe nimesema hapa kwamba hii ni ramadhani ya sita its six ramadhan they are spending in lockup hata kesi haijaanza kushughulikiwa six years shame on this country, shame on our system. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnatuambia tusiseme nje, tunaitukana nchi yetu humu ndani shame kwa nchi yetu, shame kwa Serikali zetu kwamba miaka sita mtu anachunguzwa hata kesi aijaanza jamani fikirini hata kesi haijaanza fikirini jamani wale binadamu kama sisi next it could be you, it could be mwanao, it could be mtu mwingine, jamani watu wanasema sheria haina huruma miaka sita inatosha jamani, inatosha, inatosha, inatosha miaka sita. Waamulieni kama wana makosa waukumuni hakuna mtu anayesema anaunga mkono ugaidi, nataka kama ugaidi miaka 50 mia 200 wafungwe lakini wawe wameukumiwa kesi i-move, kesi haija-move mnataka nini tuambieni halafu mnasema mna tunza haki nyie watetezi wa wanyonge ninyi its rubbish, hamfanyi chochote kwa haki ya nchi hii. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ally Saleh unayemwambia rubbish ni nani? Hebu mimi nakuheshimu sana hebu tumia ile lugha ya Kibunge tu, futa hiyo kitu.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni aibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ya mwisho namalizia juu ya habari ya kichakaa, kichakaa ni kama utani kule pemba kuna msemo mmoja umesema uchumi wa mudu, uchumi wa panga, panga hutumika kwa kukatakata vitu vingi kulima kufanya nini lakini mwisho hutupwa lisionekane mpaka msimu ujao. Ni sawa sawa na hawa polisi wetu manawatumia katika uchaguzi, mnawatumia katika operation, mnawatumia kuzuia mikutano yetu lakini vyeo vyao hamuwapi haki zao hamwapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, polisi wa nchi hii wanatumika vibaya wanatumika visivyo lakini haki yao basi minimum wapeni haki zao, wapandisheni vyeo kwa wakati sio kwa kuwa hawana pa kusema, sio kwa kuwa wanapiga salute hawa mabwana wanaitikia mkaona hawasemi wanatuambia mnawafanyia vibaya hamuwapi haki zao hata tukisema mara nyingi polisi wa nchi hii wana lala pabaya hawana mahali pa kulala hawana matunzo mengine yanayostahiki askari jamani vibayeni wanasema wapemba vibayeni, vibayeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.