Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. DANIEL N. NSANZUGWAKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Labda nianze moja kwa moja kwa kuwapa hongera sana viongozi katika Wizara hii, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, na makanda wote wa Jeshi la Polisi hongereni sana. Lakini kwa namna ya pekee na chukua nafasi hii kumpongeza RPC wa Mkoa wa Kigoma ndugu Otieno na ma-OCD wake kwa kazi kubwa wanayoifanya kule Kigoma ukizingatia Kigoma ni Mkoa wa mpakani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri na wewe binafsi nikushukuru kwa kufanya ziara katika Mkoa wa Kigoma na hasa Wilaya ya Kasulu ulikuja tukakutembeza maeneo mbalimbali ukaenda mpaka Kitanga ukashuhudia mauaji yaliyotokea hongera kwa kazi, na karibu sana katika Mkoa wetu wa Kigoma.

Labda Mheshimiwa Waziri nikukumbushe jambo moja, Mkoa wa Kigoma unapakana na nchi nne ndiyo mkoa pekee katika nchi hii ambao unapakana na nchi nne, unapakana na Zambia upande wa maji, unapakana na Congo DRC, tunapakana na Burundi na Rwanda. Na nchi zote hizo Mheshimiwa Waziri unajuwa ukiacha tu nchi ya Zambia nchi zilizobaki DRC, Burundi na Rwanda hali yake ya usalama si shwari sana hali ni tete.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Wabunge wa Mkoa wa Kigoma tumekaa na wewe zaidi ya mara moja tukikuomba utumie mamlaka yako kwa mujibu wa instrument uliyonayo, uyatamke maeneo yenye uhalifu mkubwa ili yaweze kuwa na kikosi maalum cha polisi au mnahita kama Rorya ya Tarime ile Kanda Maalum ya Kipolisi. Na Mheshimiwa Waziri tunakusisitiza Kanda hii inaweza ikawa ni enclave ya Ngara, Biharamuro, Kakonko, Kibondo, Kasulu, na maeneo ya Buhigwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri unaposema hali ya usalama katika nchi yetu ni nzuri tena unaweka nzuri sana sisi wakazi wa maeneo yale tuna sema hali si shwari. Utekaji ni mwingi, ujambazi ni mwingi na tunaomba kabisa kabisa Mheshimiwa Waziri jambo hili mlipe kipaumbele. Nina hakika eneo hili likiongezewa rasilimali tukawa na Kanda Maalumu la Jeshi la Polisi na polisi wengine wakaendelea kuwepo katika maeneo yao hali ya usalama inaweza ikawa ni nzuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyozungumza hivi na Waziri unajuwa utekaji unaendelea katika maeneo ya Kakonko, maeneo ya Biharamuro, maeneo ya Nyakanazi, maeneo ya Kasulu, maeneo ya Kibondo na ule mpaka wetu ni mkubwa sana. Mheshimiwa Waziri ule mpaka unajuwa ni zaidi ya kilomita elfu 2000 kwa hiyo, ni muhimu sana Kanda hiyo Maalum ukaanza kufikiria na ningependa uje utueleze humu ndani mnajipangaje kuweza kupunguza uwalifu katika maeneo yale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ningependa nilisemehe ni upungufu wa askari katika Mkoa wa Kigoma, taarifa nilizonazo na wewe unazo kwamba Mkoa wa Kigoma unaupungufu wa askari kati ya 120 mpaka 150 na wewe Waziri unajuwa, wakimbizi wote wa nchi yetu wapo katika Mkoa wa Kigoma. Wakimbizi wapo Kasulu, wakimbizi wapo Kibondo, wakimbizi wapo Kakonko lakini kuna upungufu mkubwa sana wa askari pamoja na vitendea kazi. Sasa mtu yeyote mwenye akili angeweza kudhani kwa sababu Mkoa wa Kigoma upo mpakani unapakana na nchi nne hatupaswi kuwa na uhaba wa askari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haina maana unakuwa na askari wengi katikati ya nchi, unakuwa na askari wengi Dodoma, unakuwa na askari wengi Singida, unakuwa na askari wengi Tabora, unakuwa na askari wengi Shinyanga, wakati ujafunga mpaka, tafsiri yake ni nini? Tafsiri yake ni kwamba ualifu na wahalifu na silaha sinatoka nje ya nchi, zinapitia Kigoma kuingia kati kati hasa kwa akili ya kawaida nilidhani na nina amini wewe Mheshimiwa Waziri na timu yako na RPC ananisikia, RPC Sirro ananisikia haiwezekani Mkoa ambao kama shield yetu ndiyo ngome yetu tuhangaike..

MBUNGE FULANI: IGP Sirro umesema RPC.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWAKO: IGP Sirro ndiyo, aah IGP Sirro ni mtani wangu angeelewa tu hivyo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, IGP Sirro ananisikiliza haina maana nasema tena inakuwa na askari wengi katikati ya nchi, lakini kwenye mpaka ambao unaingiza silaha haramu unawakimbizi haramu, una watu chungu mzima kumeachwa wazi. Nadhani busara ya kawaida ya polisi ingetumika na wewe Mheshimiwa Waziri kwamba tufunge mpaka, ule mpaka ni mrefu sana silaha zinaingia kutoka Burundi, silaha zinaingia kutoka Rwanda, silaha zinaingia kutoka Kongo na ndiyo zinapita katikati ya nchi yetu. Sasa Mheshimiwa Waziri uioni kama ni busara kawaida tu? Ukaanza kusini mpaka kule of couse ulivyosema mkisheana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, ingawaje wanajeshi wengi walioko katika detach zile wao wanasema wanakazi yao maalum. Lakini mshirikiane kwa karibu ili mpaka ule uweze kuwa salama na wananchi wa maeneo yale tuweze kuhishi kwa amani na salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ambalo ningependa nilisemehe na msema kweli mpenzi wa Mungu nimeshangaa kwenye kitabu chako hata hukugusia ujenzi wa barracks niliokwenda kukutembeza, Mheshimiwa Waziri tumekunywa chai pale Kasulu tukaenda kutembea wewe na mimi tukaenda kwenye barracks za Kasulu. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barracks ya Kasulu ile inauwezo wa kuifadhi familia za askari zaidi ya 50 tumekwenda pale sasa nimeshangaa kwenye kitabu chako hiki hata kugusia katika miradi inayoendelea na cha ajabu Mheshimiwa Waziri zile nyumba zimejengwa pia kwa msaada wa Jeshi la Polisi, Magereza wameshiriki pale na jambo hili hata Kamanda IGP Sirro nimewai kumueleza una-priority gani kama uwezi kuhifadhi askari katika maeneo ya mipakani, kwenye kitabu chako not even a mention hata kutamka tu umeona barracks hili mambo ya ajabu haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unasema unajenga nyumba tano Kigoma, Kigoma mjini unajenga nyumba tano tunazungumzia maeneo ambayo yamekithiri kwa uhalifu, hawa askari wanakaa mitaani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitabu chako kabisa uelezi hata kutaja kwamba umetembelea barracks ile na wewe mwenyewe umeona zile blocks zile ni kubwa ni nyingi. Sasa nimeshangaa sana Mheshimiwa Waziri ningependa kwa kweli nipate maelezo kwanini? Unless ukutambua ile nguvu iliyofanyika pale kuna nguvu ya wafanyabiashara, kuna nguvu ya wananchi, kuna nguvu ya Magereza, kuna nguvu ya polisi nimeshangaa sana Mheshimiwa Waziri kwenye mpango wa maendeleo 2019/2020 hata kutaja kwamba kuna barracks inajengwa umesahau kutaja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ambalo ningependa nilizungumze ni uhamiaji tunashukuru sana Kamanda wa Uhamiaji, Kamanda wa uhamiaji tunamshukuru na wenzake na timu yake zile harassment za kutambua watu kwa sura zimepungua sana angalau zimeanza kutumia weledi. Na sisi Mheshimiwa Waziri kupitia kwako niwashukuru sana wenzetu wa uhamiaji ule umbumbu wa kutambua watu kwa sura zao eti kutambua watu kwa rafudhi zao kwa kweli vituko vile vimepungua kwa kiwango kikubwa, tunaomba waendeleze weledi, wahamiaji haramu watambuliwe kwa namna ambayo ni ya kisayansi zaidi kuliko kuangalia sura zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake sura za watu wa Congo, sura za watu wa Zambia, sura za watu wa Burundi na Rwanda zinafanana.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWAKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hiyo lakini naomba hayo yote yazingatiwe Mwenyekiti nashukuru ahsante. (Makofi)