Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo: vyombo vya habari siyo huru kabisa, haiwezi kufanya kazi yake ipasavyo. Matokeo yake Serikali haiwezi kujisahihisha na kupata maendeleo, haiwezi kujua ni wapi imekosea. Naiomba Serikali iangalie upya Sheria hiyo ya Vyombo vya Habari, kuvibaini ili visifanye kazi zake inavyostahili.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii iangalie ni namna gani inatoa elimu kwa wananchi juu ya kudumisha maadili mema. Hata walimu mashuleni, pia wazazi wafundishe maadili kwa watoto wao maana kuna mmomonyoko mkubwa sana wa maadili kwa watoto na vijana wetu.

Mheshimiwa Spika, baadhi ya mila na desturi katika makabila mbalimbali ni nzuri. Hivyo, nashauri makabila wahamasishwe kudumisha mila na desturi ambazo ni nzuri. Mfano, heshima kwa wakubwa kwa kuwapokea wakubwa mizigo au kuwaachia viti maeneo ya mikusanyiko.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali ifanye tathimini juu kutoangalia Bunge, kwa sababu watu wengi wanalalamika, hawaelewi nini kinaendelea Bungeni na kwamba hawaelewi kama wawakilishi wao wanawawakilisha vyema au la.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.