Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ZAINAB M. AMIRI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kazi kubwa anayoifanya katika Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali itenge fungu la fedha katika bajeti hii na ifike kwa wakati ili Wizara iweze kutekeleza majukumu yake kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri zetu nchini waweze kuweka utaratibu maalum wa kutoa vibali vya ujenzi za kumbi za starehe kwamba zisiwe karibu na makazi ya watu ili kuepusha usumbufu kutokana na kelele zinazotokana na shughuli mbalimbali zinazofanyika katika kumbi hizo.

Mheshimiwa Spika, ili kulinda sanaa zetu, nashauri Serikali iweke utaratibu wa kisheria utakaowezesha vituo vyote vya Radio na Television nchini kupiga muziki wa wasanii wa nyumbani kwa asilimia 70 ili pia kukuza soko la bidhaa za wasanii wa ndani.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali irejeshe viwanja vya wazi ambavyo vilikuwa vikitumika kwa michezo mbalimbali na vimebadilishwa matumizi bila kufuata utaratibu maalum.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali kutunga Sheria kali ambayo itakataza wasanii wa muziki na maigizo hususan wa kike kuvaa nguo au mavazi ambayo yanakiuka maadili na utamaduni wa Mtanzania.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali iwe na vazi rasmi la Taifa ambalo litamtambulisha Mtanzania yeyote yule awapo nje ya nchi yetu na popote pale atakapokuwa hivyo jitihada za makusudi zifanyile ili kufanikisha suala hili.