Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu kwa usimamizi mzuri wa kazi za Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kuchangia kwa maandishi na nianze kwenye michezo. Pamoja na juhudi za kusimamia michezo, kuna haja ya kuongeza bidii kwenye michezo mingine ikiwa ni pamoja na riadha, mpira wa pete, gofu na mengineyo badala ya kuweka jicho letu kwenye mpira wa miguu ambako bado tunahitaji kuweka juhudi na mikakati madhubuti ili vijana wetu waweze kucheza vizuri na pia miongoni mwao watokee makocha badala ya kutegemea makocha kutoka nje.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, kuwe na utaratibu wa kuimarisha viwanja vya michezo badala ya kuwa na viwanja vingi vya mpira wa miguu wakati kuna vipaji vya aina mbalimbali vya michezo nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali iangalie au chombo maalum kiwepo kwa ajili ya kufuatilia watangazaji, kwanza katika maslahi yao, vifaa vya uhakika vya utangazaji na mwisho kuangalia au kuchuja waandishi/watangazaji ambao hawana maudhui ya utangazaji na matamshi sahihi na fasaha ya Kiswahili.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.