Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru sana kwa kupata nafasi hii kuweza kuchangia bajeti hii ya Wizara ya Viwanda. Pia nawashukuru wapiga kura wangu, Wanamuheza kwa kuendelea kuniamini na kuweza kunifanya niendelee kuongea hapa leo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Viwanda ni Wizara muhimu sana. Ni Wizara muhimu kwa sababu inaendana na malengo ya Awamu ya Tano; wananchi wa Tanzania wengi wana mategemeo makubwa sana na Wizara hii; wana mategemeo ya mabadiliko mengi sana kwenye Wizara hii; wana mategemeo ya kupata ajira nyingi kutokana na viwanda ambavyo Awamu ya Tano inategemea kuviweka. Kwahiyo, Wizara hii ni Wizara ambayo ni ya muhimu na Wizara ambayo tunaitegemea itakuza uchumi wetu, italeta ajira nyingi na itatuondolea umaskini kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda ambavyo vilikuwepo tangu enzi za Mwalimu ni viwanda vingi, lakini vile viwanda vingi vimekufa. Sasa hivi kinachofanyika ni kutaka kuvifufua hivyo viwanda. Mkoa wa Tanga ulikuwa ni mmoja wa Mkoa ambao tulikuwa tunaongoza kwa viwanda hapa nchini.
Tuikuwa na viwanda karibu 180 na sasa hivi viwanda ambavyo viko ni 50 tu, ndiyo viwanda vikubwa na vidogo ambavyo tunaweza kusema kwamba ndio vinafanya kazi katika Mkoa wa Tanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama alivyosema Waziri kwenye hotuba yake kwamba malengo ya kwanza ni kuanza kuvifufua viwanda hivi, lakini hatuwezi kufufua viwanda hivi kama hatujajua vile vilivyokufa vilikufa kwa sababu gani. Kwa hiyo, tutakapovifufua viwanda hivi tutakuwa tunajua kwamba vile ambavyo vimekufa vimekufa kwa sababu gani, tusirudie hayo makosa tena. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Muheza ni sehemu mojawapo tulikuwa na kiwanda. Tulikuwa na kiwanda cha matunda. Matunda ambayo yanazaliwa Muheza ni matunda ambayo yanajulikana hii Afrika na ulimwengu mzima. Sisi tunaweza kutoa matunda tani 100,000 kwa mwaka. Ni matunda ambayo yanaweza kuwa ya pili au ya tatu katika Bara la Africa baada ya South Africa na Egypt.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Muheza tunatoa machungwa mengi, lakini sasa hivi hatuna kiwanda cha machungwa. Wanakuja Wakenya, wanajaa pale, wanajaza hoteli za Muheza, miezi miwili iliyopita ilikuwa ukija Muheza huwezi kupata nafasi kwasababu wamejaa Wakenya pale kuchukua machungwa yetu ku-cross kupeleka Mombasa kwenye viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nategemea Mheshimiwa Waziri, atakapokuja ku-wind up kwenye hotuba hii, atatoa matumaini ya kiwanda cha matunda cha Muheza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuhitaji kiwanda cha matunda Muheza, lakini pia tunazalisha viungo vingi kuna pilipili manga, hiliki pale baada ya Zanzibar, kuna karafuu na mdalasini. Wanakuja watu kutoka nchi za nje wanajaa Wilayani pale kwa ajili ya kuchukua malighafi hizo na kuzipeleka nje. Kwa nini tusiweke hata kiwanda kidogo pale? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ame-present hotuba yake kwa nguvu sana na inaonekana inatoka moyoni kwake. Kwa hiyo, tunategemea utekelezaji wake utakuwa ni mkubwa ili wananchi wa Muheza na wenyewe waweze kufaidika na Mheshimiwa Waziri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunategemea kwamba viwanda hivi basi vitakapozalisha vitalindwa. Nimefurahishwa sana na Mheshimiwa Rais aliposema kwamba kuanzia leo basi furniture zote za maofisini ziwe zinatokana na malighafi yetu ya humu humu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna kiwanda chetu cha kamba, kama unavyojua katani, ni zao letu kubwa Mkoani Tanga, ni zao letu kubwa Wilayani Muheza. Kiwanda cha Ngomeni cha kamba ambacho ni kiwanda kikubwa Afrika Mashariki na Kati, ni kiwanda kimojawapo ambacho watu wanalipa hela kabla hata hawajapata hayo mazao yake ambayo wanayataka pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunategemea kwamba kiwanda kile kinatakiwa sasa kisaidiwe na Serikali. Nilikwenda pale na kuongea na uongozi, wakaniomba. Wao wanaomba kitu kimoja tu, wanaomba Serikali iwape tender ya wao kutengeneza mazulia ya maofisi zote za Serikali kwenye nchi hii na uwezo huo wanao, ni suala la kubadilisha zile mashine zao pale na kuwapa mashine nyingine. Mheshimiwa Mwenyekiti, namtegemea Waziri ataweza kuwapa upendeleo kiwanda hicho, kukuza kiwanda hicho kiweze kuzalisha mazulia yote ambayo yanatengenezwa kwenye ofisi zote za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niongelee suala la EPZA. Kwanza nawashukuru sana EPZA kwa sababu wameweza kujaribu kuweka maeneo ambayo wawekezaji wakija wanaweza wakaoneshwa, ni hatua moja nzuri sana. EPZA imejikita zaidi kwenye Foreign Direct Investment (FDI). Vitu vyote wanaelekeza nje, vinapelekwa nje; vikitoka kule, vinatengenezwa, then vinarudishwa hapa hapa. Sasa nilitaka wapanue wigo wa kuweza kuwafanya Watanzania na wenyewe waweze kuelimika na kuwa wataalam na waweze kufanya vitu hivyo wao wenyewe na kuviuza hapa hapa nchini; kuleta mashine ambazo zinaweza kufanya kila kitu hapa hapa nchini na kuweza kutoa mali ambayo inaweza kuwa ni nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga tunataka tufaidike na bomba hili la mafuta la kwenda Kampala.
Kwanza tunaisifu sana Serikali kwa kuweza kupata hiyo zabuni ya kutengeneza hilo bomba la mafuta, lakini tunataka tuhakikishe kwamba tunaongeza value kwenye hilo bomba ili wananchi wa Tanga, wananchi ambao bomba hilo litapita sehemu zote, waweze kufaidika nalo. Wanaweza kufaidika nalo namna gani?
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja, ahsante.