Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Spika, Serikali ilitangaza hapa Bungeni kwamba local channels za TV zitaoneshwa kwenye ving’amuzi bure bila kulipia lakini hadi sasa zoezi hilo limeshindikana. Serikali haioni kwamba huku ni kuwanyima wananchi wa Tanzania kupata habari? Hivyo, ni vyema Serikali ikaweka msisitizo kuhusu jambo hili ambalo ni haki ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, pia, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ijenge vizuri uwanja wa mpira uliopo Mji mdogo wa Mlowo ambao ulizinduliwa na Mwenge tarehe 2 Aprili, 2019. Uwanja huu ujengwe vizuri ili kuruhusu michezo mingine iwe na miundombinu mizuri. Mfano michezo ya mpira wa pete, volleyball na michezo mingine.

Mheshimiwa Spika, ili kuboresha mpira wa miguu nchini, Serikali iangalie namna ya kuanzisha academy katika kanda mbalimbali nchini. Leo nchi nyingi zilizoendelea duniani kisoka zilianza na academy na sasa zimefikia hatua kubwa ya kisoka.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.