Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, kwanza nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa juhudi kubwa na mchango wake mkubwa katika kuinua Sekta za Michezo, Sanaa na Utamaduni.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara na Viongozi wa Wizara kwa kazi kubwa na ya uzalendo mkubwa katika kuzisimamia sekta zote za Wizara na kufikia hatua nzuri ya mategemeo kwa Taifa na wananchi. Napenda kuwatia moyo waendelee na juhudi hizo wanazozifanya, michezo na sanaa imekua na imeleta sifa kubwa kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nashauri Wizara iendelee kuendeleza vipaji vya wanamichezo pamoja na wasanii wetu sambamba na kuvumbua vipaji vipya. Serikali iendelee kuwatambua na kuwaenzi wasanii na wanamichezo kwa mchango wao mkubwa walioutoa katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kupitia vyombo na Taasisi zake zinazohusika na kutoa elimu ya maadili, viendelee kutoa elimu juu maadili mema kwa wasanii, waigizaji na wanamichezo ili waendelee kuwa kioo kwa jamii.

Mheshimiwa Spika, Kiswahili, Serikali na Wizara kwa ujumla naipongeza kwa kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili; lugha yetu hii imezidi kuzungumzwa duniani. Hivyo, nashauri juhudi hizo za kukiendeleza Kiswahili ziendelee kwa lengo la kukiongeza nguvu duniani kote, kuitangaza nchi yetu kupitia lugha yetu hiyo ya Kiswahili, kudumisha utamaduni pamoja na kuongeza soko la ajira kwa wataalam na watumiaji wa Kiswahili hapa nchini kwetu.

Mheshimiwa Spika, michezo ya zamani ambayo yana faida na mchango kwa Taifa na wanamichezo wenyewe ambayo imepotea au haina nguvu ifufuliwe na kupewa msukumo. Nashauri Serikali iongeze fedha kwa Wizara hii ili kukamilisha majukumu yao. Mwisho Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Watendaji wote wa Wizara nawapongeza kwa kazi nzuri ya kuendeleza kazi zote zilizomo ndani ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.