Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa fursa hii na nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji mzuri na hotuba yenye kusheheni mambo mazuri kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza Serikali kwa uamuzi wake mzuri wa kujenga Mahakama Kuu katika Mikoa ya Mara na Kigoma. Uamuzi huu kwa busara unaenda kutatua kero ya muda mrefu iliyopelekea wananchi wa mikoa hii kusafiri masafa marefu ili kupata huduma hii muhimu. Ombi langu kwa Serikali ni kuziwezesha Mahakama hizi kuwa na bajeti ya kutosha ili kuziwezesha kufanya kazi zake kwa ubora na ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mafia yenye vijiji 23 ina mahakama moja tu ya mwanzo, hali hii inapelekea utoaji wa huduma za kisheria kuwa mbali na wananchi. Ombi langu kwa Serikali ni kwamba, itujengee Mahakama moja ya mwanzo katika Tarafa ya Kusini kwani wananchi katika maeneo haya wengi wanatoka katika Visiwa Vidogo Vidogo vya Juani, Chole na Jibondo, wanasafiri masafa marefu na wanatumia gharama kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapitio ya adhabu na faini mbalimbali nyingi zimepitwa na wakati kulingana na mazingira ya sasa, hivyo niiombe Serikali yangu sikivu kufanya mapitio upya ya viwango vya faini na adhabu zilizopitwa na wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa nyumba ya Jaji Mkuu katika Jiji la Dodoma umekuwa ni ahadi ya siku nyingi, kiongozi wa mhimili ni vema akawa na makazi yenye hadhi sawa na wadhifa wake. Nakushukuru na naunga mkono hoja.