Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hoja ya Waziri wa Katiba na Sheria kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya Mwenyekiti wa Mahakama ya Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; kumekuwa na ucheleweshwaji wa kazi za ardhi na migogoro kutokana na kutokuwepo kwa Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi. Tunaomba Tunduru tupatiwe Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi ili kupunguza migogoro ya ardhi inayozidi kuongezeka siku hadi siku katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa majengo ya Mahakama; kuna upungufu mkubwa wa majengo ya Mahakama. Katika Jimbo la Tunduru Kusini, hivyo shughuli nyingi za Mahakama kufanyika katika maeneo yaliyofanana na Mahakama. Pamoja na kutokuwepo kwa nyumba za Mahakimu wengi na Mahakimu wanakaa katika nyumba za kukodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Mahakama; kumekuwa na upungufu mkubwa wa Mahakama. Jimbo la Tunduru Kusini lina Tarafa tatu, Nalasi, Hukumbule na Namasakata na Kata 15, lakini Mahakama zinazofanya kazi hazizidi tatu, moja kila Tarafa, hivyo tunaomba angalau kila Kata kungekuwa na Mahakama ya mwanzo ili kupunguza migogoro ya wananchi wetu huko vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu mkubwa wa Mahakimu; Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina upungufu mkubwa wa watumishi wa Mahakama (Mahakimu) pamoja na Makarani wa Mahakama, hivyo tunaomba tuongezewe Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo ili kurahisisha kusikiliza kesi mbalimbali. Mahakama zilizopo hazina Mahakimu na kufanya Mahakimu waliokuwepo kuwa na mzigo mkubwa wa kusikiliza madai mbalimbali ya wateja hivyo kufanya Mahakimu kufanya mzunguko kupita kusikiliza kesi katika Mahakama zilizopo vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa vitendeakazi; Mahakama zilizopo Tunduru zina changamoto kubwa ya vitendeakazi hasa magari na pikipiki. Mahakimu waliopo hawana hata vyombo vya kusafiria ili kwenda kusikiliza kesi vijijini, hivyo kufanya kesi kuahirishwa mara kwa mara kutokana na kutokufika kwa Hakimu kusikiliza kesi hizo kwa kukosekana usafiri.