Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuchangia.
Jambo la kwanza nitumie fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Rais, ameongelea suala la sukari huko alikokuwa anaelekea Arusha, kwa sababu jambo hili ni jambo la dharura, ni jambo kubwa, kwa sababu leo tu pale Choma cha Nkola sukari ni shilingi 5,000, Nzega Mjini ni shilingi 4,000, Igunga Mjini ni shilingi 3,200, Kibaha hapo kwenye mzani ni shilingi 3,000.
Kwa hiyo, naiomba Serikali, alichokisema Mheshimiwa Rais huu mchakato wa kuagiza sukari na sukari kuingia nchini, kwa sababu mwezi wa Ramadhani umebaki siku chache na kwa tabia ya soko bidhaa huwa zinapanda sana na moja ya bidhaa ambayo huwa inapanda ni sukari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kumwambia kaka yangu Mwijage, mimi nitakuunga mkono leo. Bajeti hii nitakuunga mkono, ila ya mwaka kesho ukija kwa style hii sitakuunga mkono. Nasema hivi kwa sababu moja, ukisoma ripoti ya Kamati ya Viwanda na Biashara katika miradi ya kimkakati iliyotajwa na Mheshimiwa Waziri, moja ni kufufua General Tyre. Serikali inataka kutenga two billion, lakini Kamati inasema ili uifufue General Tyre unahitaji shilingi bilioni 60. Bajeti ya Serikali ni bilioni 80! Kwa hiyo, namwonea huruma Mheshimiwa Mwijage, anaenda kufanya muujiza gani? Mimi namtakia kila la kheri. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivi? Ukisoma hotuba ya kaka yangu Mheshimiwa Mwijage, page namba 43 mpaka 49 anasema uendelezaji wa viwanda vya kimkakati. Kiwanda cha kwanza nachokitaja ni Kiwanda cha Makaa ya Mawe cha Mchuchuma na Liganga ambacho CAG amesema mkataba wake una harufu ya ufisadi, strategic partnership tunayotaka kufanya na hawa Wachina, ina walakini. Nasema namtakia kila la kheri kaka yangu, Mheshimiwa Mwijage.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa pili ni wa Magadi Soda wa Engaruka; mradi wa tatu ni wa Viwatilifu TAMCO Kibaha. Najiuliza swali dogo, nimeamua kwenda hadi kwenye dictionary kutafuta tafsiri sahihi iliyotajwa katika Mpango wa miaka mitano, lakini vilevile iliyotajwa na Mheshimiwa Mwijage, ya nini strategic industries? Strategic industries kutokana na dictionary ya Cambridge inasema kwa kiingereza, nanukuu; “an industry that a country considers very important for economic development.” Hii ndiyo tafsiri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, I am asking myself, kama tunataka kuuondoa umaskini wa nchi hii, ni wapi pa kuanzia? Engaruka? General Tyre? Ukisoma Mpango alichokisema ukurasa wa 62, flagship project, kipengele cha kwanza, anasema maamuzi ya uwekezaji yote yatakuwa based on the countries comparative advantage.
Mheshimiwa Mwenyekiti, my question is, do we have comparative advantage over others in the world, kwenye uwekezaji huu wa kutengeneza matairi? Hili ni swali najiuliza namtakia kila la kheri kaka yangu Mheshimiwa Mwijage. Huo muujiza mwaka kesho niuone. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulisema wakati tunachangia Mpango Bunge lililopita, nchi hii 65% ya wananchi wetu wako kwenye sekta ya kilimo, kwa nini Processing Industries? Ninayo hotuba ya kaka yangu Mheshimiwa Mwigulu, nendeni page namba 23 pamba; mwaka 2013/2014 uzalishaji ulikuwa 245,000; mwaka 2015/2016 uzalishaji ulikuwa 149,000, una nosedive! Uzalishaji unaporomoka! Tumbaku uzalishaji unaporomoka! Kila sehemu uzalishaji unaporomoka. What are we doing?
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kosa letu la kwanza, ni utangulizi wa kauli yetu ya Mpango wa mwaka mmoja; hili ndilo kosa la kimkakati tulilofanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema hivi, naomba ninukuu; “Mpango unakusudiwa kuwa na maeneo ya vipaumbele vinne, viwanda vya kuimarisha kasi ya ukuaji uchumi, miradi mikubwa ya kielelezo, miradi wezeshi kwa maendeleo ya viwanda ikiwemo barabara, reli, nishati, bandari, maji, mawasiliano, maendeleo ya viwanda; maeneo yatakayolenga kufungamanisha maendeleo ya viwanda na watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema tunataka maeneo yatakayofungamanisha maendeleo ya viwanda na watu, halafu hayo maeneo hatuwekezi. Hatuwekezi kwenye pamba, hatuwekezi kwenye katani, hatuwekezi kwenye korosho, hatuwekezi kwenye alizeti, hatuwekezi popote, halafu tunatarajia muujiza! Nawaombeni Mawaziri, ushauri wangu wa kwanza kwenu, Mheshimiwa Waziri Mwijage kwanza in your mind, wewe ni mtoto, ni matokeo ya wengine. Mkae mtengeneze strategic unit ili muongee lugha moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia hotuba ya Mheshimiwa Mwigulu, nimeangalia ya kwako, nimekata tama. We are planning to fail kaka zangu! Hatuwezi kujadili kufanya revolution kwenye uchumi wa nchi hii bila kuamua kuweka vipaumbele vya maeneo yanayogusa watu. Tutakuja hapa kusema uchumi wetu umekuwa kwa asilimia nane, umaskini bado upo kwa sababu mipango yetu yote inaacha watu wetu wengi nje. Hakuna inclusion! Hatuwa-include watu wengi kwenye mipango yetu; na hili ni tatizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia uwekezaji, nataka nikwambie Mheshimiwa Waziri, nenda kwenye database ya Wizara, miaka minne iliyopita kilo moja ya ngozi, raw, kwa mchunaji machinjioni ilikuwa shilingi 3,000 leo ni shilingi 400.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakutana mwaka kesho, namuunga mkono kaka yangu.