Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la haki za binadamu kwa nchi yetu ya Tanzania ni wimbo wa mdomo, lakini kiutekelezaji hakuna kabisa. Ni miaka 58 tangu nchi yetu ipate uhuru, lakini katika maeneo ya mahabusu, Vituo vya Polisi na Magereza nchi nzima haki za binadamu hakuna kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia suala la haki za binadamu, tunagusa mambo mengi ikiwemo kusikilizwa, kutibiwa, malazi na sehemu ya kujisitiri kiafya. Hadi leo wanajisaidia mahali pa wazi huku wengine wanamwona. Isitoshe sehemu wanayojisaidia na chakula wanalia hapo hapo na kulala hapo hapo. Kutenda kosa kunamwondolea mtu kuwa siyo binadamu. Naomba Mheshimiwa Waziri anapohitimisha hoja hii atoe majibu, ni lini sasa suala hili litakoma?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasikitika kuwa hotuba ya Katiba na Sheria katika kipindi ambacho Taifa linapitia katika changamoto ya kutoheshimu utawala wa sheria, ni kipindi ambacho Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na sheria mbalimbali za nchi na kanuni zake hazifuatwi; ni kipindi ambacho matamko yasiyozingatia tena Katiba, sheria na kanuni yanatolewa hadharani kwenye majukwaa ya siasa na wakati mwingine hutolewa kwa waraka bila woga wowote; ni kipindi ambacho dira ya ofisi nyingi za Serikali imejielekeza inafanya nini ili mtu afurahi zaidi. Kwa maneno mengine, dira ni kumfurahisha mtu zaidi kuliko kuzingatia matakwa makuu ya katiba na sheria za nchi yetu.