Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hadi sasa Tanzania haina Tume Huru ya Uchaguzi, naiomba Serikali kuunda Tume Huru ya Uchaguzi ili kutenda haki na kudumisha demokrasia ya kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Katiba ya sasa ina upungufu mwingi, mfano muundo mzima wa kupata uongozi unaondoa uhalali wa Katiba hiyo. Hivyo, naiomba Serikali iendeleze mchakato wa kupata Katiba mpya maana kipengele kilichobaki ni kupiga kura kwa Katiba hiyo mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na kutokutenda haki kwa Mahakama zetu nchini. Mahakimu wengi wamekuwa wakifuata maelekezo ya Serikali katika kutoa haki badala ya kusimama kama mhimili unaojitegemea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.