Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria na watendaji wote kwa kuleta hotuba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika eneo la urejeshwaji wa wahalifu wa kimataifa katika makosa ya jinai (P.36). Tanzania inapakanana nchi za jirani za Maziwa Makuu. Kwa mfano,Mkoa wa Kigoma umepakana na nchi jirani za Congo DRC, Rwanda na Burundi. Kuna matukio mengi ya kihalifu yanayohusishwa na raia wanchi jirani kuvuka mipaka kuingia Tanzania na kufanya uhalifu kwa kupora mali za wananchi, kuteka, kubaka na wakati mwingine kufanya mauaji. Matukio kama haya yanatokea Kakonko, Kobondo na Kasulu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine nashawishika kuamini kwamba wahalifu hao wa kigeni wanao wenyeji wanaowawezesha kuingia na kutoka nchini bila kutiwa nguvuni. Je, Wizara inazo taarifa za wahalifu wa kigeni (wakiwemo wakimbizi) katika Mkoa wa Kigoma ambao wamerejeshwa nchini ili wajibu mashtaka? Katika eneo hili, naishauri Wizara kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani hususan Polisi na Uhamiaji ili kudhibiti wimbi la uhalifu unaoaminika kutekelezwa na wenyeji kwa kushirikiana na wageni ambao inasemekana wakishavuka mipaka kwenda kwao hawapatikani kwa urahisi kuja kujibu mashataka yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.