Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani iliyosomwa na Mheshimiwa Salome Makamba kwa niaba ya Mheshimiwa Lisssu Antiphas.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mlimba lenye Kata 16, Serikali imeanza ujenzi waMahakama ya Mwanzo, Kata ya Mlimba na jengo limefika juu (boma). Ingawa boma limeisha mwanzoni mwa Machi 2019 lakini vibarua wa ujenzi ambao ni wakazi wa Mlimba ambao idadi yao yapata 19 hivi hawajalipwa. Je, huyo mkandarasi hajalipwa hadi ashindwe kulipa waliofanya kazi? Naomba mkandarasi huyo afuatiliwe na awalipe vijana hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali ilete marekebisho ya Sheria ya Polisi kukamata watuhumiwa walioachiwa na Makahama na hapo hapo Askari Polisi kuwakamata kwa kutumia kifungu 225. Kifungu hicho kimepitwa na wakati kwani kinasababisha mlundikano wa mahabusu kwenye magereza na vituo vya polisi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri viongozi wa Wizara hii watembelee magereza nchini na magereza zote zaMkoa wa Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kuwepo muda maalum wa kuchunguza kesi za jinai nchini kwa kuwa magerezani kumekuwa na wananchi wengi na wanakaa muda mrefu hadi miaka 10 mahabusu kusubiri kukamilika kwa upelelezi. Upo ushahidi usio na shaka kwa mahabusu wengi kusota maregeza muda mrefu kwa kuwa hawana msaada wa kisheria na pesa za kutoa rushwa kwa wapelelezi. Nashauri mtembelee magereza na kuongea na mahabusu ili mpate taarifa muhimu zinazohusu rushwa.