Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa namna ya pekee naomba nipongeze mhimili wa Mahakama kwa kufanya kazi vizuri. Hata huo mrundikano wa kesi tunaouona ni kwa sababu watu wana imani kubwa na mahakama na ndiyo maana wanakwenda kupeleka mashauri yao. Hapa nimeona complain kubwa katika Kitabu cha Hotuba ya Kambi ya Upinzani wanasema mahakama haina uhuru, yaani kama mahakama inaingiliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhuru wa mahakama umeanzia kwenye Katiba ibara ya 107B, ambayo inasema: “Katika kutekeleza mamlaka ya utoaji wa haki, mahakama zote zitakuwa huru na zitalazimika kuzingatia tu masharti ya Katiba na yale ya sheria ya nchi.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kuipa mahakama uhuru wake umeanzia kwenye Katiba, lakini wenzetu wanashindwa kutofautisha kati ya Mahakama za Hakimu Mkazi, wanawapongeza Majaji kama sio sehemu ya mahakama. Utaratibu wa maamuzi ya mahakama ya chini kupelekwa katika Mahakama ya Rufaa ni utaratibu wa kimahakama; uwe umeshinda au umeshindwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo wao hawaziamini mahakama za chini lakini wanawapongeza Majaji, hawajui Majaji na wenyewe ni sehemu ya mahakama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, limeongelewa suala la Katiba. Kupanga ni kuchagua. Hata baba anapopata hela nyumbani matatizo yapo mengi anaamua na ndiyo maana hata wao hela ya ruzuku inapopatikana wanaamua kukopeshana Wabunge kununua magari; japokuwa hawana ofisi wanashindwa kujenga ofisi, wanakopeshana Wabunge kununua magari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kuendelea kudumisha utawala wa sheria na Katiba pamoja na kuboresha sheria mbalimbali. Tumeshuhudia Sheria ya Madini imefanyiwa marekebisho, sheria ambayo ilikuwa kandamizi. Pia Sheria ya Vyama vya Siasa ambayo ilikuwa kandamizi ambapo ilikuwa inatoa mianya ya baadhi ya Wenyeviti ruzuku inapopatikana wanaolea mke wa pili na watatu badala ya kufanyia vitu vingine vya vyama. Sheria za Mitandao, sisi viongozi ni waathirika wakubwa sana wa sheria mbovu za mitandao ya kijami. Tulikuwa tunashuhudia Wabunge, wanamziki na watu maarufu wanazalilishwa. Kwa hiyo, naipongeza Serikali kwa kuweka sheria kali za mitando ili kukomesha tabia hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Statistics, jana hapa tulishuhudia Mheshimiwa Mbunge akisema Mkoa wa Tabora peke yake wanafunzi waliopewa mimba kwa mwaka mmoja ni 70,000. Takwimu hizi zinaenda kwa watu huko, watu wengi hawasomi wengi wanapata data kutokana na kusikiliza. Sasa sheria zikiwa mbovu watu watakuwa wanapata taarifa ambazo siyo sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Vyombo vya Habari, vyombo vya habari zimekuwa nguzo kubwa ya kuzalilisha watu na kutoa taarifa za uongo. Kwa hiyo, hata sheria kali zilizowekwa sitasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa upotoshaji mkubwa ambao unafanywa na vyombo vya habari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, Mheshimiwa Mbunge mmoja ameomba uwekwe utaratibu katika Katiba Maalum juu ya upatikanaji wa Viti Maalumu vya Wanawake. Navyofahamu mimi kila chama kimepewa mamlaka ya kuteua Wabunge wa Viti Maalum. Kwa mfano, CCM kuna makundi ya wanawake mikoani wanachaguana wenyewe mikoani, vyuo vikuu, vijana na walemavu. Kwa hiyo, kila kundi limeweka utaratibu wake wa kuwapata kwa kupigiwa kura. Sasa wenzetu wana utaratibu wao ambapo wameachia watu wachache wanafanya huo uchaguzi na ndiyo maana umeona analalamika kuwa Mheshimiwa Polepole amewasema vibaya lakini hao hao wanalalamika kwa Katiba haijasema wanapatikanaje.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)