Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, kauli za wanasiasa zinakua kikwazo katika ustawi wa Mazingira yetu. Sheria ya mita 60 kama ikifanywa kama siasa na kuruhusiwa kuharibu vyanzo vya maji, itakuwa kiama kwa nchi yetu, kwani itaharibu mazingira, kusababisha upotevu wa mvua na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vipi vifungashio vya mikate, ni sehemu ya katazo hilo? Kwa nini tusitoe muda maalum kwa wazalishaji hawa? Naomba ku-declare interest kwamba mimi nazalisha mikate na kutumia mifuko hiyo. Bado hakujawa na mbadala sokoni na wafanyabiashara washanunua mizigo na hata kubadilisha mashines.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ije itusaidie kutengeneza kingo za bonde la Mto Msimbazi kwani bonde linazidi kukua na kutafuna majengo na makaazi ya watu. Tunaomba Wizara itoe kipaumbele kwa mto huu. Tunawaombeni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishati mbadala kama gesi zishushwe bei hata kupunguza kodi ili wananchi wengi watumie gesi badala ya kuni na mkaa kama ilivyo sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vikundi vya akina mama viwe motivated na Wizara. Wale wanaozalisha mkaa mbadala binafsi, naikaribisha Wizara kutembelea mradi wa akina mama wa Tabata wanaozalisha mkaa mbadala. Karibu mtunishe mfuko wao waweze kupata mashine ya kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara isaidie wabunifu kubuni zaidi mashine za kuzalisha mkaa mbadala.