Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu kubwa kwa Mheshimiwa Waziri wa Mazingira ni namna Wizara inavyoachia mifugo hasa ng’ombe kuharibu mazingira yetu kwa kiwango kikubwa. Mkoa wa Lindi ni moja ya mhanga mkubwa wa hali hii; mifugo inaingia bila kuzingatia uwezo wa mazingira yaliyopo katika eneo husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Lindi ipo hatarini kugeuka jangwa. Jimbo langu la Mchinga ni kielelezo cha hoja hii. Wafugaji wanavamia maeneo yote oevu ya Jimbo la Mchinga kama vile bonde la Mbwenkulu na eneo la bonde la Mkoa lililopo katika Kata za Mvuleni na Kitomanga. Wizara lazima ishirikiane na Wizara ya Mifugo katika kupanga maeneo mbalimbali hapa nchini. Uchungaji holela wa mifugo yetu utapelekea kuligeuza Taifa letu kuwa jangwa siku chache zijazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ya pili ni kuhusu miti adimu ya mikoko na mkakati wa nchi wa upandaji mikoko. Kutokana na umuhimu wa miti hii, Serikali inapaswa kuongeza juhudi katika kuilinda na kuongeza miti ya mikoko.