Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ENG.CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Makamu wa Rais, Waziri na wasaidizi wenu wote kwa kazi nzuri katika masuala ya Muungano na Mazingira. Kipekee, naipongeza Serikali kwa hatua yake ya kuondoa mifuko ya plastiki sokoni ifikapo tarehe 31 Mei, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika maeneo matatu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania siyo kisiwa. Kwa kuwa nchi nyingi zilizoendelea zinaratibu matumizi mazuri ya mbegu za GMO, nashauri wataalam waendelee kufanya utafiti wa kitaalam hususan kwenye mbegu za mazao zinazotumia teknolojia ya GMO ili kujua faida na madhara yanayotokana na teknolojia hiyo badala ya kuchukua uamuzi wa jumla wa kuikataa teknolojia ya GMO. Kwa mfano, utafiti umeonesha kuwa uzalishaji wa pamba kwa kutumia teknolojia ya GMO umeongezeka maradufu katika nchi zinazozalisha pamba kwa GMO (Wizara ya Kilimo wanazo takwimu).

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiongeza uzalishaji wa pamba tutawezesha upatikanaji wa malighafi kwa ajili ya viwanda vya nguo tunavyoanzisha sasa. Hata hivyo, kutakuwa na haja ya kufanya utafiti wa kina kuhusu matumizi ya mafuta ya kula yanayotokana na pamba itakayozalishwa kwa teknolojia ya GMO.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi makubwa ya maji ni yale ya kilimo cha umwagiliaji kwa sababu consumptive use ya mimea inayomwagiliwa ni kubwa kuliko matumizi ya nyumbani (domestic use), viwandani na yale ya miradi ya kuzalisha umeme ambayo consumptive use ni sawa na hakuna kwa sababu karibu maji yote yanayotumika kuendesha mitambo yanarudishwa kwenye mto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kushirikiana kwa karibu na Wizara inayohusika na kilimo cha umwagiliaji na Wizara ya Maji, makampuni makubwa ya miwa (sukari) na mashamba makubwa ili wazingatie mambo muhimu yafuatayo:-

(a) Matumizi sahihi ya maji kwa mazao husika (crop water requirements) na water rights ili kuepuka matumizi makubwa yanayosababisha vyanzo vya mito kukauka.

(b) Kulinda uharibifu wa ardhi kwa chumvi na kuwa na kilimo endelevu. Kila mradi wa umwagiliaji, hasa ile ya flooding iwe na miundombinu ya kutoa maji ya ziada shambani (drainage systems) kwa sababu ukosefu wa miundombinu hiyo husababisha chumvi kuongezeka (salinity) na ardhi inaharibika. Gharama za kurejesha ardhi inayoharibika kwa salinity ni kubwa sana.

(c) Usimamizi wa sheria nyingine zinazoshabihiana na Sheria ya Mazingira, mfano Sheria ya Rasilimali za Maji ya 2009. Wenye viwanda vinavyotumia maji ni lazima waheshimu sheria hii pamoja na sheria nyingine. Katika miaka ya 1990, kulikuwa na mgogoro mkubwa kwenye Kiwanda cha Karatasi Mjini Moshi (Kibo Pulp and Paper Board). Tatizo lilianza pale ambapo kiwanda kilipewa water right kwa ajili ya kutumia kiwandani kuzalisha karatasi. Katika kiwanda hicho, matumizi mengine yalikuwa ya kemikali ya aluminium sulphate ambayo ina sumu (toxic).

Sheria ya Rasilimali Maji iliwataka wenye kiwanda kujenga mtambo wa kusafisha maji (treatment plant) kabla ya kuyarudisha maji katika Mto Karanga baada ya kuyatumia kiwandani. Kiwanda hakikufanya hivyo badala yake kilichepusha maji katika mfereji na kuwapelekea wakulima wa mpunga. Matokeo yake yalikuwa mawili; moja, wakulima waliwashwa na sumu ya Al (SO ) ; pili, mazao ya mpunga yalipungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana suala hili lilisharekebishwa kwa sababu wanamazingira waliingilia. Ushauri wangu ni kwamba sheria zote ambazo zinashabihiana na utunzaji wa mazingira, zisimamiwe vizuri na zieleweke kwa ngazi zote katika Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.