Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mungu kunipa fursa hii ili nitoe mchango wangu kwenye eneo hili la mazingira. Utunzaji wa mazingira ni muhimu sana kwa uhai wa binadamu. Utunzaji wa misitu, vyanzo vya maji, usafi wa mazingira ni sehemu ya uhai wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita zaidi kwenye utunzaji wa misitu kwa sababu ndiyo chanzo kikubwa kinachovuta mvua, hivyo kupata maji ya mvua kwa ajili ya kilimo na vilevile maji kwenye mito, maziwa kwa ajili ya ustawi wa jamii. Bado Serikali haijawekeza vya kutosha katika utunzaji wake. Tumeshuhudia misitu ambayo imetunzwa kwa muda mrefu ikikatwa kiholela. Tumeshuhudia makazi yakijengwa au shughuli za kibinadamu katika misitu mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli wananchi wengi bado wanatumia nishati ya kuni na mkaa kwa matumizi ya nyumbani, ni kweli pia kwamba uchomaji mkaa umekuwa changamoto kubwa katika kuteketeza misitu na watumiaji wengi wa mkaa wanaishi mjini. Ni kwa nini sasa Serikali hii ya Awamu ya Tano isifanye maamuzi magumu kwa kutoa ruzuku kwenye mitungi ya gasi iliyojazana mjini ili kuwezesha watumiaji wengi waweze kununua mitungi hiyo kwa bei nafuu sana na kuachana na matumzi ya mkaa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kuna usambazaji wa gesi asilia kwa baadhi ya makazi na viwanda mbalimbali lakini zoezi hili ni la muda mrefu sana mpaka kuja kusambaa eneo kubwa la nchi. Utatuzi wa haraka wa kuinusuru misitu yetu na vyanzo vya maji ni matumizi ya mitungi ya gesi ya majumbani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni matumaini yangu kwamba Serikali itachukua hatua ili kunusuru mazingira na uhai wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.