Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kabla sijaanza kuchangia kwanza niweke rekodi maana naona Wabunge wa CCM wakisimama wanaanza kufanya reference kwa chaguzi ambazo zilifanyika 2015 kurudi nyuma. Tuingize kwenye rekodi tu kwamba Marais waliotangulia hawakuwahi kutamka bayana kwamba Wakurugenzi Watendaji ambao wameteuliwa na yeye wasipomtangaza mtu wa CCM watakuwa hawana kazi, hawajawahi kutamka bayana, lakini Rais Mheshimiwa Dkt. Magufuli ametamka bayana na amenukuliwa na vyombo vyote. Kwa hiyo tukisimama hapa tukiongea inabidi wakae wakemee, vinginevyo wataingiza nchi kwenye machafuko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niingize kwenye rekodi kwamba Makatibu Mezani mnapunja sana muda wa upinzani. (Makofi)

WABUNGE FULANI: Kweli hiyoo, kweli hiyoo.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti wa Chama ameongea chini ya dakika saba na hajawa interrupted, sisi tulikuwa tunamrekodi hapa tunaomba muwe fair kabisa maana yake wote tuna-deserve muda wa kuongea hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja hii ambayo ni muhimu sana kwenye mustakabali wa nchi yetu. Tumekuwa…

NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tena kwa mujibu wa…

MWENYEKITI: Ni kuhusu utaratibu.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, umemkatalia Chief Whip hapa..

MWENYEKITI: Kwa mujibu wa kanuni gani Mheshimiwa?

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tena nirudie kwa mujibu wa kanuni ya 64 kwamba Mbunge hatatoa maneno ya uwongo katika Bunge. Ninalotaka kusema ni kwamba namwomba mchangiaji aliyekuwa anakaa sasa hivi kwa sababu anamzungumzia Mheshimiwa Rais ambaye tunaamini kwamba anaamini katika uchaguzi na kwa maneno hayo aliyozungumza yaingie kwenye rekodi, ningeshauri yasiingie kwenye rekodi wakati yeye hajaleta uthibitisho wa hayo maneno aliyozungumza Mheshimiwa Rais.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Matiko, endelea kuchangia. (Makofi)

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Tumekuwa tukishuhudia Mawaziri wanakuja wanaeleza wananchi kwamba uchumi wetu unakuwa kwa asilimia saba, yaani tumekuwa tukieleza uchumi wa nchi unakuwa kinadharia zaidi kuliko kiuhalisia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona kabisa taarifa ya Shirika la Fedha Duniani imesema bayana kwamba uchumi wetu unakuwa kwa asilimia nne. Uchumi kukua tunaupima vipi, moja ya kigezo ni kuangalia pia na kiwango cha umaskini cha watu wetu wananchi. Ukiangalia kiwango cha wananchi wa Tanzania awamu hii…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Matiko, wewe ni Mbunge mzoefu sana ili ujenge hoja yako vizuri kuhusiana na ukuaji wa uchumi wa Tanzania kile kinachodaiwa na IMF ungelikuwa nacho hapa, unasema hiki hapa nakiweka hapa unaendelea kuchangia.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ulinde muda wangu ukitaka document…

MWENYEKITI: Narudia kama unayo just lay on the table, unaendelea kuchangia

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, I will lay it on the table right, I don’t have it now, but I will do that.

MWENYEKITI: Very good, ahsante.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukuaji wa uchumi unapimwa pia kwa kuangalia umaskini wa wananchi wetu. Ukiangalia Serikali ya Awamu ya Tano pamoja na kwamba sikatai lakini imejiegemeza sana kwenye maendeleo ya vitu badala ya maendeleo ya watu. Ukiangalia hata kwenye mpango hapa wameainisha bayana kabisa kwamba ili kuweza kufikia uchumi wa kati kichwa chao mojawapo watawekezwa kwenye maendeleo ya watu. Maendeleo ya watu namaanisha elimu, afya, maji, kuhakikisha wanawawezesha wananchi wao kiuchumi kupitia uwekezaji na vitu vingine lakini ukiangalia kiuhalisia Serikali inafanya kwa kiwango kidogo sana katika kuhakikisha kwamba inaweka maendeleo kwa wananchi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kwenye elimu, tumeshuhudia elimu yetu ambayo mmesema mnatoa elimu bure…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Nimeshakataa taarifa Waheshimiwa.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshuhudia kwamba tumeendelea kuona watoto wetu wanasoma kwa kurundikana wanafunzi 200 wengine wanasoma kwenye miti. Tumeendelea kuona Walimu wakiwa wana-work load kubwa kinyume kabisa na uwiano wa mwanafunzi kwa Mwalimu. Tumeendelea kushuhudia ajira hazitolewi kwa Walimu. Tumeona juzi wametangaza ajira 4,000 tu lakini watanzania zaidi ya 91,300 wame-apply kwa ajira 4,000 tu ambazo zimetolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia, ningeomba kuweka kwenye kumbukumbu, Mheshimiwa Waziri alivyoleta taarifa hapa angetuambia upungufu wa Walimu ni kiasi gani, lakini ameonyesha tu kwamba Walimu waliopo mwaka jana tumeajiri kiasi fulani, sasa hivi tunategemea kuajiri kiasi fulani. Tusipowekeza kwenye elimu, Taifa ambalo haliwekezi kwenye elimu kamwe halitakaa liendelee. Haya mambo tunayoyajenga sijui Stieglers Gorge, SGR, nimeenda juzi pale Kinyerezi naambiwa hata wale wanaokuja kufanya maintenance pale inabidi watoke nje kuja kufanya maintenance ya vifaa vile vya Kinyerezi, ina maana vikiharibika mitambo mingine ibebwe ipelekwe nje hii yote ni kazi, inabidi tuwekeze kwa watu wetu ili waweze kuja kuwa wanahudumia hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia statistically kwa Tarime tu mwaka jana nikiwa gerezani niliona watoto waliofaulu kwenda form one wengi wameachwa. Nilitarajia kuona Serikali ingewekeza kuhakikisha kwamba inamalizia maboma yote ambayo yamejengwa na wananchi. Kwa mfano Tarime wananchi walijitolea wakajenga maboma 40 kwa shule za sekondari na tukaandika kuja wizarani ili tuweze kupata fedha, hatukuweza kupata fedha za kumalizia maboma 40.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika halmashauri za Mkoa wa Mara Tarime Mji na Bunda Mji ambapo mapato yetu ni madogo sana hatukuweza kupata hata senti tano ya kumalizia maboma ili watoto wetu waweze kwenda sekondari na waweze kusoma. Kwa hiyo utanona kwamba kipaumbele cha Serikali ni kuwekeza kwenye vitu badala ya kwenye maendeleo ya watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia pia kwenye afya ni the same hata kama tumejenga vituo mia tatu na kitu. Nashukuru Nkende nimepata kituo kimoja, lakini bado tatizo halimaliziki, tunahitaji kuenga vituo vya afya, tunahitaji mahospitali yawe na dawa, vitendanishi na wataalam, waajiri Madaktari wa kutosha, tunahitaji kuona kwamba Mtanzania mfanyabiashara, mkulima wanakuwa na afya bora kuweza kufanya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kusema tu kwamba kwa Tarime Mji ile hospitali tunahudumia Rorya, Serengeti na wengine, lakini mnatupa fedha za basket fund kama vile ni watu wa Tarime Mji, watu 78,000. Tunaomba mkiwa mnatoa fedha muweze ku-consider kwamba tuna work load kubwa. Vilevile Daktari wa Kinywa na Meno wa Tarime alifariki lakini mpaka sasa hivi hatujapata replacement, wananchi wetu wanahangaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie vitambulisho vya wajasiriamali, wamevizungumzia pamoja na kwamba vimeathiri ushuru kwa maana ya kwa halmashauri zetu mapato yanapungua, lakini nataka nijue zaidi. Hivi vitambulisho tunaambiwa kwamba vimetengenezwa Ikulu, vimetengenezwa na Rais, nataka nijue vitambulisho hivi vimetengenezwa kutoka fungu gani, maana yake sina kumbukumbu kama tulishawahi kupitisha fungu hapa kwa ajili ya kwenda kutengeneza hivyo vitambulisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia je, hivi vitambulisho vimefuata Sheria ya Manunuzi ya Umma, Na.7 ya mwaka 2011 na 2016? Je, walishindanisha tenda? Mzabuni ni nani aliyeshinda kutengeneza hivi maana yake mwisho wa siku atakuja atapita CAG, halafu itakuja Audit quarries tujue. Mbaya zaidi hivi vitambulisho ambavyo wanasema laki sita wanaovitoa ni Ma-DC ambao sio Maafisa Masuuli. Kwa hiyo, hii inaacha maswali mengi sana na wananchi wanasema badala ya Chama cha Mapinduzi kupeleka zile milioni 50 kama walivyoahidi kwa kila kijiji, ila sasa wameenda tena kuwakata wale maskini elfu 20 kujaza mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua, je, hivi vitambulisho ni chaka ambalo linakusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao au ni nini? Tunaomba watuondoe huo wasiwasi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Tarime ni Mji ambao unakua, tunahitaji taa za barabarani, hata Mheshimiwa Rais alivyopita alisema mji ule unakua. Kama ambavyo wameweka Lamadi, tunaomba na Tarime nako waweze kutuwekea taa za barabarani. Uteuzi wa Wakurugenzi tumeukemea hapa na tutaendelea kuukemea kwa mujibu wa sheria inatakiwa angalau Mkurugenzi anayeteuliwa awe ametumikia kwenye utumishi wa umma angalau miaka mitano, lakini tumeshuhudia wakurugenzi wanaoteuliwa ni makada. Mfano wa juzi tu wa somebody Mhagama, alikuwa ni Katibu wa CCM kateuliwa kuwa Mkurugenzi, wanaziua halmashauri zetu kuleta watu ambao hawana, lazima tufanye succession plan kwenye halmashauri zetu. Wateue ma-DC ambao ni makada wao lakini kwenye kada ya Ukurugenzi, wazingatie sheria. (Makofi)