Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA:Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa nafasi hii ili nami niweze kutoa mchango wangu katika Wizara hii ya TAMISEMI. Kwanza nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijalia afya njema lakini pia kuweza kusimama hapa leo jioni hii. Pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kwa hotuba yake nzuri, lakini pia tumpongeze sana kwa kazi nzuri anazozifanya. Vile vile niwapongeze Manaibu Waziri, niwapongeze watendaji wote wa Wizara hiyo kwa kazi nzuri wanazozifanya, lakini vile vile nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Utumishi na Utawala bora, hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee kabisa nimpongeze sana Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, nimpongeze Waziri Mkuu na Mawaziri wote kwa jinsi wanavyotekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi. Hongera sana.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo nianze kutoa mchango wangu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali kwa jinsi ilivyojipanga kuhakikisha afya za Watanzania zinaimarika vizuri. Kwa kweli Serikali imejitahidi kwa kiasi kikubwa sana kuweza kujenga hospitali za wilaya, hospitali za mkoa lakini pia kujenga vituo vya afya, zahanati, kununua vifaa tiba vya kutosha na kikubwa zaidi kupata madawa ya kutosha kwa nchi nzima. Haya yote ni matunda mazuri ya Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. John Pombe Magufuli, tunamshukuru sana, tunampongeza mno na tunamtakia kila lililo la kheri katika maisha yake hapa duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wangu wa Geita tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais na tunaishukuru sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi tumeweza kupata billion 5.9 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya rufaa na kwa sasa tumeshapata bilioni 3.7 na mkandarasi yupo kazini anaendelea. Tunaishukuru sana Serikali na tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, palipo na mafanikio lazima kuna changamoto; changamoto yangu ya kwanza ni upungufu wa Wauguzi katika zahanati zetu, kuna upungufu mkubwa sana wa watumishi katika zahanati zetu, unaweza ukakuta zahanati moja, ina Muuguzi mmoja,anafanyaje kazi. Sasa niiombe sana Serikali iweze kuona ni namna gani itaweza kutupatia Wauguzi wa kutosha katika zahanati zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya pili ni upungufu wa Madaktari katika vituo vyetu vya afya. Hili pia ni tatizo, huko kwenye vituo vya afya tunapofanya ziara, kuna vituo vya afya vingine utakuta daktari mmoja na muuguzi mmoja. Kituo cha afya ni wananchi kata nzima, wananchi hawa ni wengi mno kuweza kupewa huduma na mtu mmoja, niiombe sana Serikali iweze kuona ni namna gani itaweza kutupatia Madaktari wa kutosha katika vituo vyetu vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto yangu ya tatu ni kukosekana kwa Madaktari Bigwa katika wilaya, niiombe sana Serikali yangu iweze kupeleka Madaktari Bigwa kwa watoto na akinamama katika hospitali zetu za wilaya. Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu kumekuwa na msongamano mkubwa mno kwenye hospitali zetu za rufaa kwa sababu ya wagonjwa wengi kwenda kwenye rufaa, lakini Madaktari Bigwa wakiwa kwenye hospitali za wilaya tutapunguza huo msongamano na wananchi wetu watakuwa hawapati shida kama hivi sasa. Naomba sana Mheshimiwa Waziri aweze kuliona hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine tena, katika Mkoa wangu wa Geita wananchi wamehamasika sana kujenga maboma kwa ajili ya vituo vya afya lakini pia, Zahanati kwa maana hiyo tunamaboma mengi sana ambayo yamesimama na nimpongeze sana Mkuu wangu wa Mkoa wa Geita kwa jinsi alivyosimamia ujenzi huo, niombe sasa Serikali iweze kuunga mkono jitihada za wananchi hawa ili maboma hayo yaweze kukamilika kwa kuezekwa na wananchi hawa waweze kupata huduma hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kumaliza hayo, naomba kuunga mkono hoja.Ahsante.(Makofi)