Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Naam!
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuzungumza kidogo. Naomba nizungumzie kwamba kama tunataka kutengeneza nchi ya viwanda ili twende kwenye uchumi wa kati mimi nafikiri kiwanda ni matokeo ya uwekezaji katika umeme. Lazima tuwe na umeme utakaoweza kufanya viwanda vifanye kazi. Kwa hiyo, niishauri Serikali kwamba ijitahidi sana kuwekeza katika umeme ili tuwe na umeme wa uhakika. Tukiwa na umeme wa uhakika viwanda ambavyo tunataka vije ama tuvifufue basi viweze kupata uwezo wa kufanya kazi vizuri. Huo ulikuwa ni ushauri wa kwanza. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, nizungumzie hoja hii ya sukari. Tanzania kuna viwanda vinne ambavyo vinazalisha sukari. Kuna kiwanda cha Ilovo, kipo Jimboni kwangu Kilombero, kuna kiwanda cha Mtibwa, kuna cha TPC na kuna Kagera. Kiwanda cha Ilovo kimefunga uzalishaji wake tangu mwezi wa kwanza na hii ni kwa sababu ya maintenance, lakini leo ajabu karibu tani nane za sukari kutoka Ilovo zilikuwa kwenye godown hapo Tabata zimeuzwa leo. Hili godown lipo Tabata limeuza tani nane. Tafsiri yake ni nini? Tafsiri yake ni kwamba tuna sukari ambayo imefichwa na wafanyabiashara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Rais akiwa na nia safi, mimi nasema safi kwa sababu anazungumza vizuri ya sisi tuweze kupata sukari na viwanda viendelee, watu wanaficha sukari, wanasubiri maintenance za viwanda zikifanyika wao ndiyo watoe mzigo. Kibaya zaidi baada ya huu upungufu wa sukari hawa watu wanataka wapewe vibali vya kwenda kuagiza sukari yaani watu wanaoficha sukari kwenye ma-godown leo wanataka wao ndiyo wapewe vibali vya kwenda kuagiza sukari. Tafsiri yake ni nini? Tafsiri yake ni kwamba hao watu kwa tabia yao hii ya kuficha kwanza hatuna uhakika kama wataagiza ambacho wameruhusiwa, maana yake ni kwamba wataongeza. Wakiongeza viwanda vyetu hivi vinne vya Ilovo, Mtibwa, TPC na Kagera vikianza production vitakuta tayari kuna mzigo mkubwa upo kwenye soko vitapunguza uzalishaji. Vikipunguza uzalishaji maana yake hawa wakulima wetu mfano wakulima wangu kule Sanje, Kidatu, Mkula wataathirika. Tunakwenda kuua hawa wananchi ambao wanaendesha kilimo hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu sasa, niiombe Serikali isiruhusu kabisa wafanyabiashara waagize sukari nje. Mimi najua kuna watu wamewekwa humu ndani waweze kuongea maneno haya, wamewekwa humu ili waweze kusema kwamba wafanyabiashara waruhusiwe, niombe Serikali, hivi viwanda vinne na kwa sababu Serikali hii inaweza sana, hawa Mawaziri wanafanya kazi bila kuwa na sheria, hawana kazi, basi niombe kama huo ndiyo utaratibu wetu hata kama viwanda hivi watasema kwamba sijui havina mamlaka haya, tuendelee hivi hivi tu, tufunike hivi hivi hawa wenye viwanda, viwanda hivi ndiyo viagize sukari ili kulinda viwanda hivi na wakulima. Nilikuwa nataka hili niliweke sawa watu wajue na Serikali ijue kwamba kuruhusu wafanyabiashara binafsi kuagiza sukari ni kuua viwanda na kuuwa wananchi watu wa Sanje na sehemu zingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu Morogoro. Morogoro ina viwanda vingi sana lakini viwanda hivi watu wanafuga mbuzi, hapa ndipo wanaposema we have killed our past and we are busy killing our future. Tumeua past yetu na tuko busy kuua future yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi huwa najiuliza hivi nia ya Serikali ya privatization (kubinafsisha) hivi viwanda ilikuwa ni nini? Ilikuwa ni kuwapa watu nafasi ya kupata maeneo ya kufuga, kuuza mashine zetu kama scraper au nia ilikuwa tuongeze uzalishaji na ajira?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nia ilikuwa ni kuongeza ajira na uzalishaji hivi inakuwaje tunakuwa na viwanda yaani kama Taifa tumejiminya, tumepata viwanda, tukasema wenzetu mviendeleze halafu wanachukua hivyo viwanda wanaanza kufugia mbuzi, wanakata mashine, wanauza kama scraper, kama Taifa hii ni aibu! Sidhani kama Serikali hii ya Awamu ya Tano inayosema Hapa Kazi Tu itaruhusu kwamba hizi ndizo kazi zenyewe. Yaani kazi ya Mwalimu Nyerere ilikuwa kuunda viwanda halafu watu wengine waje kukata scraper! Sidhani kama hii ndiyo kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo mifano hapa, pale kwangu Mang‟ula pana kiwanda kinaitwa MMT, nina handover letter hapa ambayo hii Serikali ilikabidhi hiki kiwanda kwa Mama Rwakatare, Mama Rwakatare huyu huyu ambaye alikuwa Mbunge, handover hii hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu walikuwa hawajui kama mlikuwa mnaona vifaa kama mapanga na kadhalika vyenye picha ya mamba ilikuwa ni Mang‟ula. Kiwanda tumekabidhiwa kikiwa kizuri, kikiwa kina kila kitu lakini pale sasa hivi kuna mbuzi tu ndiyo wanachungwa pale lakini unakuta eti mtu naye anajiita mwekezaji, amewekeza nini huyu? Umewekeza kwa kuua uchumi wa nchi? Kile kiwanda kilikuwa kinatoa ajira pale, Serikali ikaamua kutoa, ikasema endeleza na nimuombe Waziri twende kule akaone kiwanda hiki ambacho kilikuwa kina manufaa katika nchi yetu leo kimekuwa cha kufunga mbuzi. Hatuwezi kujenga Taifa la hivi na tukiongea hivi hatumuonei mtu, tunaongea ukweli kwa sababu ya faida ya Taifa letu. Kuna watu huko hawana ajira, tumetoa viwanda watu wanafugia mbuzi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo kama haitoshi, kuna kiwanda kingine kilikuwepo pale Mang‟ula, wengine mnafahamu vizuri wakati reli hii ya TAZARA inajengwa vifaa vya kutengeneza yale mataruma vilikuwa pale Mang‟ula. Mwalimu Nyerere kaacha viwanda vizuri, kiwanda vya Ilovo, kiwanda vya Mtibwa spare zake ilikuwa wanazipata Mang‟ula. Leo kiwanda mtu anachukua semi-trailer anapakia chuma chakavu anapeleka kuuza, sisi tupo tu hapa, Taifa lipo, Serikali ipo! Kiwanda kinahujumiwa, nchi inaliwa tunasema wawekezaji, what kind of this business? Are we serious?
MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: We are not serious and never be serious. We have killed our past and we are busy killing our future. Ukiuliza, anaongea mpinzani, anaongea UKAWA, come on lets be serious! Tunazungumzia uchumi wa nchi hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri twende tukaone kule! Kiwanda ambacho mnasema mmempa mtu mkaone…
MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.