Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mawaziri na watendaji wote kwa kuleta hotuba hii. Napenda kuchangia maeneo mawili, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzishwa kwa Mfuko wa Kinga ya Bei za Mazao (Price Stabilization Fund). Eneo hili limechangiwa pia na Mheshimiwa Bashe. Nilitamani kumpa taarifa lakini nikaamua kuleta mchango kwa maandishi. Kati ya miaka ya 2012 – 2014, Wizara ya Kilimo ilianzisha mchakato wa kuanzisha Price Stabilization Fund kwa mazao ya korosho, kahawa, pamba na tumbaku kwa lengo la kukabiliana na madhara yanayotokea pindi bei ya mazao zinapoanguka hasa katika masoko ya dunia. Sijapata habari kwa nini mchakato huo haukuendelezwa au kama uliendelezwa ulifikia hatua gani. Nashauri Mheshimiwa Waziri alipeleleze suala hili, inawezekana bado lina umuhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maafa yako ya aina mbalimbali kama vile njaa, ukame, moto, matetemeko, mafuriko na kadhalika. Leo napenda kuchangia suala la maafa yanayotokana na mafuriko. Mafuriko yanapotokea yanaathiri mazao, miundombinu kama ya biashara, reli, nyumba na kadhalika. Yako maeneo yenye mito ambayo mara kwa mara inaleta mafuriko yanayoharibu madaraja, barabara, reli, simu na kadhalika kama kule Kilosa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ijipange kujenga mabwawa makubwa ambayo yatakuwa na manufaa makubwa mawili. Kwanza kuepusha uharibifu wa miundombinu na pili yatumike kwa kilimo cha umwagiliaji wakati wa kiangazi. Suala hili linahitaji utayari wa kukabiliana na majanga, je, Serikali inao mkakati wa disaster preparedness? Hasara ambayo Serikali inapata kutokana na gharama za kurudishia miundombinu inayohabiriwa na mafuriko ni kubwa lakini pia uharibifu unapotokea unasababisha fedha na rasilimali nyingine kuelekezwa katika ukarabati wa miundombinu badala ya kuelekezwa kenye maeneo (miradi) mipya ya maendeleo.