Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha maoni yangu kwa maandishi kuhusu hoja ya Waziri Mkuu. Awamu hii ya Tano, hali ya kisiasa si shwari sana kama tunavyoaminishwa. Utamaduni ulioanza kujengeka wa kubana Vyama vya Upinzani visishiriki siasa kwa uhuru kwa kusingizia taarifa za kiintelejinsia ilhali Chama Tawala wanaandama, wanaitisha mikutano ya ndani bila shida yoyote. Nia hii ovu ya double standard inachochea uvunjifu wa amani na kujenga chuki kubwa baina ya Chama Tawala na Vyama vya Upinzani, kinyume kabisa na maono na kazi kubwa aliyoifanya Baba wa Taifa kujenga mshikamano wa Kitaifa kwamba sisi wote ni ndugu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kukamata Wapinzani na raia na kuwajaza mahabusu kwa uonevu na kuwanyima dhamana ni hatari kwa amani na usalama wa nchi. Wizara husika ihakikishe kesi za mahabusu zinasikilizwa na haki kutendeka kwa kuachiwa kwa dhamana au kuhukumiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni ushiriki wa sekta binafsi. Mimi nilikuwa Kiongozi aliyesimamia reforms Serikalini na katika reforms hizo ni dhana ya Public Private Partnership (PPP) kwa masikitiko makubwa nimeona jinsi dhana hii ya PPP ilivyoachwa kabisa. Miradi mingi ya ujenzi wa majengo ya Serikali wanapewa taasisi za Serikali, ni kama kutoa fedha kutoka mfuko wa kulia na kuhamisha mfuko wa kushoto kwenye suruali hiyo hiyo. Matokeo yake sekta binafsi imesinyaa, Serikali inasahau kwamba sekta binafsi inaposhamiri ndiyo inatoa ajira kwa wingi kuliko Serikali. Serikali isishangae kuona vijana wengi wasio na ajira, hii Serikali ya Awamu ya Tano ndiyo inayosababisha. Serikali ya Awamu ya Tano irejee kwenye Blueprint ya Awamu zingine na kuziendeleza, vinginevyo tutakuwa tunarudi nyuma kila Serikali mpya inapoingia madarakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.