Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kutumia wasaa huu kukushukuru wewe kwa kunipa nafasi ya kuchangia Hotuba ya Waziri Mkuu kwa Bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nitumie nafasi hii kumpongeza sana Waziri wetu Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa kwa juhudi zake chanya katika mchakato mzima wa utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa miaka mitano. Waziri wetu Mkuu huyu amekuwa akitekeleza majukumu yake kwa ufanisi na unyenyekevu mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu katika bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu utajikita katika sehemu mbili; bandari kwa masaa ya mchakato wa uagizaji mafuta na usambazaji wake na suala zima la biashara ya magari, hasa bonded warehouse.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2012 kilianzishwa chombo kilichokuwa kinaitwa Petroleum Importer Coordinator (PIC) ambapo chombo hiki baadaye kilivunjwa na kuanzishwa PBPA Wizarani ikiwa na majukumu ya kusimamia uagizaji wa mafuta na ku-discharge mafuta kwa wasambazaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo shida katika Taifa letu, shida hii lazima kama Taifa Bunge letu litimize wajibu wake kuishauri Serikali kwa maslahi ya nchi. Serikali yetu ina umiliki wa asilimia 50 katika Kampuni ya Tipper lakini vita inayoikumba kampuni hii utashangaa. Inawezekanaje tunaagiza mafuta nje ya nchi, yakifika Dar es Salaam kila importer anapelekewa mafuta moja kwa moja kwenye deposit yake wakati tunayo Tipper, chombo ambacho kina capacity kuhifadhi mafuta yote ya nchi hii na yaliyopo kwenye transit? Tipper wanapigwa vita eti wanaiba mafuta, sisi tumerogwa na nani? Serikali tuna hisa fifty percent Tipper ina maana Serikali tunaiba mafuta?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaiba mafuta against nani? Tunawaamini zaidi importers wakiwemo Engen, Oryx, Oilcom, Lake Oil kuliko chombo hiki cha umma ambacho tukiweza kuwa na one au single terminal receiving matanki ya Tipper yana uwezo wa kuhifadhi mafuta lita milioni 220, sawa na capacity ya kupakua meli tatu kwa wakati mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tipper ambayo ni sehemu ya Serikali ikipewa jukumu la kusambaza mafuta yote ya Oil Marketing Companies (OMC) wanaweza kusambaza mafuta ndani ya siku tatu baada ya ku-deliver na jambo hili linaweza kufanyika ndani ya siku sita tu kwenye depots. Ni muda muafaka sasa Tanzania kuepuka ujanja na wizi unaofanywa na wafanyabiashara wa mafuta kwa kupiga vita single terminal receiving.

Mheshimiwa Mwenyekiti, single terminal receiving ya mafuta ndiyo mfumo pekee unaotumika duniani kote. Hata mafuta ya transit wanunuzi wa nje ya nchi watachukulia mafuta kutoka Tipper na hivyo kuliingizia Taifa mapato na pia kuisaidia TRA kukusanya mapato yake kutoka eneo moja tofauti na practice ya sasa ya kufuatilia mapato kutoka kwa OMC moja moja kutoka depots zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, damage charges tunazoingia kwa meli kuwa katika foleni, OMC wanalipia wastani wa dola 25,000. Dola 25,000 USD kwa siku, sasa unajiuliza kama hakuna ujanja kwa nini tunafifisha efficiency kwa chombo ambacho Serikali tunaweza ku-monitor uingiaji wa mafuta na usambazaji na kuliingizia Taifa ajira.

Mheshimiwa Waziri Mkuu najua yeye ni mzalendo na mtu wa haki, weka historia katika nchi hii kwa kuhakikisha kuanzia leo mafuta yote yanayoagizwa nchini yanamezwa na Tipper na waagizaji wote wapeleke kwenye deposits zao toka Tipper.

Mheshimiwa Mwenyekiti, faida za kuwa na single receiving terminal ni hizi; moja, hapatakuwa na damage sababu meli zitaweza kumwaga mafuta kwa wakati. Mbili, ili kuepuka wizi au diversion ya mafuta mabomba ya mafuta kati ya SBM na Tipper itenganishwe; na tatu, tutaongeza wigo wa Transit Cargo Consignment.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wetu Mkuu na Serikali wajue kwamba wafanyabiashara wanapoteza wastani wa shilingi milioni 330 kwa gharama za demurrage kwa wastani wa siku @25,000 USD kila meli inapokuja kupakua mafuta, wastani wa call za vessel za mafuta ni 24 kwa mwaka, hivyo wastani huu unapelekea kupoteza pesa karibu 19,776,970,608 kila mwaka zinapotea sawa na wastani wa milioni 824,040,422 kwa kila shipment.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge hili ni kazi yake kuishauri Serikali, ni wakati muafaka katika majumuisho ya hotuba ya Waziri Mkuu Serikali sasa wakubali kufanya mabadiliko ya haraka kwa maslahi mapana ya nchi yetu kwa kuifanya Tipper iwe mpokeaji na msambazaji wa mafuta yote ya nchi kutoka kwa petroleum traders.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo wa sasa kwa upakuaji wa mafuta bandarini una kasoro kubwa na unatia walakini wa ukweli wa idadi halisi ya mafuta yanayoingizwa nchini kwa mfano kwa idadi ya terminal 18 – saa kati ya 36- 54 zinapotea kutokana na kuhamisha umwagaji kutoka terminal moja kwenda nyingine. Taifa letu tuna shida moja tunalalamika sana, tunatengeneza vitu vizuri lakini hatutaki kutekeleza wakati mwingine kwa viongozi wetu kupotoshwa kwa makusudi au kwa kutokujua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tipper ni chombo ambacho Serikali yetu ina umiliki, ukifanya analysis ya kimapato nje ya gawio, Serikali imepata revenue karibu asilimia 68 kutoka Tipper moja kwa moja, Serikali tunapata revenue ya almost 70% kutoka Tipper na oryxy mbili anachukua asilimia 30% tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya ushauri huu, naiomba Serikali yangu sikivu ya CCM kuanza mara moja matumizi ya single terminal receiving. Naunga mkono hoja.