Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu na Waheshimiwa Mawaziri na watendaji wote katika Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kazi nzuri na hasa usimamizi wa Serikali na miradi mikubwa ya maendeleo. Hata hivyo ninayo mambo yafuatayo kama ushauri:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya ufundi, kwa kuwa Serikali imejikita katika uchumi wa viwanda ni lazima irejeshe elimu ya ufundi ya mafundi sadifu (technicians), sasa hivi Serikali inajikita kuandaa mafundi mchundo (artizans) kutoka VETA. Mfumo huu wa elimu unaacha ombwe kati ya mfumo wa utendaji kazi za ufundi, Mhandisi mmoja kutoka vyuo vikuu, Mafundi Sadifu 25 kutoka vyuo vya ufundi na Mafundi Mchundo 15 kutoka VETA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, waajiri sekta binafsi wanalipa tozo ya SDL ya 4.5% iliyolengwa kupelekwa VETA kuongeza ujuzi wa wafanyakazi, lakini fedha hizo hazipelekwi zote, sehemu kubwa inapelekwa vyuo vya elimu ya juu kwa wanafunzi, siyo wafanyakazi, waajiri wanaona kuwa hii si sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, waajiri wanaamini kuwa lilikuwa kosa la kiufundi kuiweka VETA chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, VETA ilistahili kuwa chini ya Wizara ya Kazi na Ajira, chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa sababu VETA ililenga kuongeza ujuzi wa wafanyakazi.