Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, uwekezaji dhidi ya kazi/ajira; pamoja na jitihada za Serikali kuifanya TIC kuwa chini ya Ofisi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, bado kuna jitihada inapaswa zitazamwe katika suala zima la welfare ya wafanyakazi katika maeneo yaliyowekezwa. Wafanyakazi hawalipwi ipasavyo, hakuna social security, hakuna utaratibu wa bima za afya, kimsingi ustawi wa wafanyakazi katika sekta binafsi ni eneo linalopaswa kutazamwa kwa ukaribu na wenzetu wa kazi na ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watumishi wa umma wakati wa uhakiki wa watumishi, wako ambao kimakosa waliondolewa kwenye mfumo na baadaye walirejeshwa. Hata hivyo hawajalipwa malimbikizo yao ambayo kimsingi mamlaka husika zimeshayathibitisha, isipokuwa ni Hazina kufanya malipo. Suala hili hakika linashusha morali ya watumishi, nashauri na kupendekeza Hazina walipe malimbikizo hayo kwa kuwa ni makosa ya kibinadamu ambayo yamerekebisha ni muafaka sasa wa kulipa malimbikizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme; Mafinga kutokana na viwanda vingi Mji wa Mafinga nimeshauri mara kadhaa nishati (TANESCO) watazame kwa macho mawili pawepo na Wilaya ya ki-TANESCO ya Mafinga maana pia Mufindi kama Wilaya ina Viwanda vingi vya Chai, Karatasi Mgololo, hivyo uhitaji wa umeme ni mkubwa sana kutokana na mazao ya misitu. Nashauri kuwa uwekezaji tunaovutia uendane na upatikanaji wa umeme wa viwandani maana kadri uzalishaji unavyoongezeka ndivyo na ajira na mapato zaidi.