Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naunga mkono hoja hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Ukurasa wa 25 wa hotuba, unatoa takwimu za miradi mipya ya uwekezaji mpaka Februari 2019 kuwa 145. Ningetaka kujua ni mingapi mpaka sasa imeanza kujengwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeongea na baadhi ya wawekezaji ambao wamelalamikia mlolongo wa vikwazo au taratibu ambazo si rafiki kwa wawekezaji wanaokuja na mitaji yao. Kupata kibali au leseni inachukuliwa muda mrefu. Nashauri Serikali ipitie upya taratibu na hatua zilizopo ili tuvutie zaidi wawekezaji waje Tanzania badala ya kwenda kwa nchi za jirani. Kwa mfano, tunaweza tukaamua uwekezaji wa kujenga kiwanda, mlolongo wote wa hatua za kuchukuliwa zikamilike ndani ya Taasisi moja (one center) na kila hatua ipewe muda maalum (that is time factor) na uwepo ufuatiliaji wa kila hatua ili kujua sababu za mkwamo na hatua za kuchukuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwekezaji wa viwanda vinavyochakata mazao ya wakulima na wafugaji vipewe kipaumbele kwani hivi vitainua uchumi wa wananchi na kutoa ajira. Yupo Mwekezaji wa kujenga kiwanda cha kuchakata matunda ya maparachichi kinachotarajiwa kujengwa Wilayani Wanging’ombe (OLIVADO CO) amekuwa anazungushwa karibu amekata tamaa, nataka kujua ni lini atapewa leseni ili ajenge kiwanda hicho?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa na tatizo la soko la matunda ya parachichi kwa muda mrefu na baada ya mwekezaji huyu kuja tumehamasisha wananchi wetu kulima zao hili la parachichi, naomba sana Serikali itumie nguvu iliyokuwa nayo ili kiwanda hiki kijengwe mapema.