Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wakulima vijijini wanapata tabu sana kuhangaika kulima chakula chao, matokeo yake hawafanikiwi kutokana na wanyama kuingia mashambani wakavuruga mazao hayo, jambo ambalo linawarudisha nyuma kuendelea na harakati zao za maendeleo. Napenda kuishauri Serikali kuwa, wafugaji wanaofanya vitendo hivi wachukuliwe hatua stahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma za jamii kama elimu; Serikali inatekeleza kikamilifu mafanikio ya elimu licha ya juhudi za Serikali wanazozifanya, kuna watu wachache wanarejesha nyuma Serikali yetu hasa uvujaji wa mitihani nchini. Kuna sehemu mitihani ilichelewa kufanywa, nishukuru Serikali yangu kwa jitihada zake, mithani imeendelea kufanywa, lakini napenda kuishauri Serikali suala hili waliangalie kwa kina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajira na vijana; nguvu kazi za vijana ni muhimu sana kuwezeshwa nchini, asilimia yao wanayopata wanaifanyia kazi kubwa lakini changamoto zao katika kazi zao ni kwamba hawana soko madhubuti la kuuza vitu vyao. Sasa basi, naomba Serikali Tukufu ilione suala hili na iwapatie soko la uhakika ili waondokane na tatizo hili . Sasa nimpongeze Waziri Mkuu na watendaji wake kwa jitihada nasema asanteni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja na naomba kuwasilisha.