Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mungu, mwingi wa rehema na wakati wote nitaendelea kuwashukuru wazazi na wapigakura wangu wa Jiji la Tanga kwa kuniwezesha kuwa Mbunge wao. Nitaendelea kuwawakilisha katika kufikisha kero zao katika Bunge letu ili ziweze kufanyiwa kazi na kuwapelekea wananchi maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya vijana; vijana wote ndio engine ya maendeleo na nguvu kazi katika sekta zote iwe ajira, michezo, kilimo, uvuvi, viwanda na kadhalika, mfano, vijana wana nguvu ya kusukuma mbele shughuli za kiuchumi. Ajira viwandani wanaajiriwa viwanda kwa kuwa wana nguvu ya kuendesha mashine kubeba na kutengeza mashine na kupakiwa bidhaa na kupeleka maeneo mbalimbali ya nchi. Hivyo nadiriki kusema vijana Taifa la leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zamani wanafunzi walikosa nafasi kuendelea na masomo kidato cha kwanza na kidato cha tano na sita, walikuwa wanajiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na waliweza kupata mafunzo ya ufundi umeme, uashi, seremala na vifaa vya kielektroniki kama computer, magari na kadhalika. Baada ya kufuzu mafunzo yao, waliweza kujiajiri na kuweza kupata kipato cha kujikimu kimaisha. Nashauri vijana walioondolewa masharti magumu kujiunga na JKT.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walemavu, nichukue fursa hii kumpongeza agizo la Serikali na pia kusisitiza kuwa utaratibu wa kutenga 10% ya mapato ya Halmashauri zote nchini kwa magawanyo zifuatao 2% watu wenye ulemavu, 4% vijana, 4% akina mama. Nashauri mgawanyo huu usimamiwe kikamilifu na fedha zitolewe kwa wakati ili kufikia malengo tuliojiwekea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya kiuchumi ukurasa II, pato la Taifa lilikuwa kwa 6.7 mwaka 2018 badala ya 6.2 mwaka 2017 ukiangalia wananchi watanzania mitaani wamechoka wako hpi bi taaban mzunguko wa fedha ni mdogo, benki hazikopeshi, masharti ya mikopo ni magumu sana, hali inayopelekea wananchi kukopa katika VICOBA, BRAC, SEDA, Poverty Africa, FINCA na kadhalika ambazo zinatoza riba kubwa sana kiasi kupelekea wakopaji kunyang’anywa vyombo vyao, nyumba zao kupigwa mnada.

Mheshimiwa Mwenyekiti, thamani ya shilingi kuporomoka; thamani ya shilingi ya Tanzania kila kukicha imekuwa ikiporomoka/kushuka kwa thamani (inflation), lakini tunaambiwa uchumi unakua, naomba ufafanuzi katika hili kwa faida ya Watanzania. Mfano, mwaka 2018 USD moja ilikuwa sawasawa na shilingi 2226 mpaka mwaka 2019 USD moja ni sawasawa na Sh.2400. Mwaka 2018 pound moja ilikuwa sawasawa na shilingi ….. mpaka mwaka 2019 pound moja ni sawasawa na shilingi…. Mwaka 2018 shilingi moja ya Kenya ilikuwa sawasawa na shilingi 20 mpaka mwaka 2019, shilingi moja ya Kenya sawasawa na shilingi 220. Mwaka 2018 S/Rand moja ilikuwa sawasawa na shilingi…mpaka mwaka 2019 S/Rand moja ni sawasawa na shilingi ….. Katika hali hii ambapo shilingi ya Tanzania inashuka uchumi unakuwaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumuko wa bei, ulipungua kwa wastani 4.0%, mwaka 2018 hadi 3.0 mwaka 2019 mwezi Januari. Sasa nataka nipate ufafanuzi kwa kuwa naona ipo tofauti katika taarifa kwa mfano ufuatao:-

(i) Mwaka 2018 Juni – Sukari kilo moja ilikuwa shilingi 2,100 lakini mwaka 2019 sukari kilo moja ni shilingi 2,500;

(ii) Mwaka 2018 Juni –Maharage kilo moja yalikuwa Sh.1,700, lakini mwaka 2019, maharage kilo moja ni Sh.2,400;

(iii) Mwaka 2018 Juni –Tambi zilikuwa kilo moja Sh.1,800, mpaka mwaka 2019, tambi kilo moja ni Sh.2,500;

(iv) Mwaka 2018 Juni – mafuta yalikuwa lita moja ni Sh.1,100, mpaka kufikia 2019, mafuta lita moja Sh.2,000; na

(v) Mwaka 2018, petrol lita moja ilikuwa Sh.1,600, lakini mpaka kufikia mwaka 2019, petrol lita moja ni Sh.2,206.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu hii hapo juu mfumuko wa bei Tanzania umeshuka au umezidi? Waziri atoe ufafanuzi kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya elimu na sintofahamu kwa wazazi, Katika sekta ya elimu kuna sintofahamu hasa baada ya Serikali kutangaza elimu bure darasa la kwanza hadi kidato cha nne. Wazazi wanaelewa kuwa bure ni free no charge, hivyo hawalipii maji, umeme, mlinzi, uji na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaeleza kwa kila mwezi inatoa fedha katika sekta ya elimu Sh.… kwa mwezi, wananchi wanajua fedha za Serikali ni nyingi na zipo. Hali imepelekea umeme na maji kukatwa shuleni (mkumbuke Mheshimiwa Rais aliwaambia TANESCO, penye deni la umeme kata na pia ulinzi hakuna na vifaa shuleni vimeanza kuibwa. Ushauri, naomba Serikali itolee ufafanuzi elimu bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Jamii NSSF, LAPF, LPF, PSPF, PPF na wafanyakazi. Mifuko hii inakusanya mapato kupitia makato yanayokatwa katika kipato cha watumishi mbalimbali Serikalini na sekta binafsi na Mfuko mmoja PSSF lakini bado kuna tatizo pale wastaafu wanapodai mafao yao baada ya kustaafu kuna usumbufu mkubwa sana. Kama tunavyojua ukistaafu mategemeo ni akiba yako (mafao ya kustaafu). Hivyo nashauri na kuomba Waziri aeleze usumbufu huu chanzo chake nini na usumbufu huu utakwisha lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, upo utaratibu umefanyika wa kuwaongezea pension waliokuwa watumishi wa Serikali toka Sh.50,000 hadi Sh.100,000 lakini kwa waliokuwa watumishi wa Mashirika ya Umma (SU), bado watumishi wa SU wanaendelea kulipwa pension ya Sh.50,000 kwa malimbikizo ya malipo baada ya miezi mitatu (3). Tukumbuke wastaafu ni watu wenye umri mkubwa na wana shida na matatizo mengi. Ushauri wangu ni kwamba, waliokuwa watumishi (SU) waongezewe na wao toka Sh.50,000 hadi Sh.100,000 na walipwe kila mwezi bila malimbikizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya kisiasa nchini ni ngumu na demokrasi inahitaji kuboreshwa na kuimarishwa. Kitendo cha kuzuia mikutano ya hadhara na maandamano kumepelekea msisimko wa kisiasa na uelewa wa siasa kwa wananchi kurudi nyuma au kupunguza hamu na ladha ya siasa hadi kupelekea baadhi ya wanasiasa kupotea katika ramani ya siasa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapomzuia mwanasiasa asifanye mikutano ya hadhara, asifanye maandamano, ni sawa na kumzuia mkulima asiende shambani, mvuvi asiende baharini, mchezaji asiende uwanjani au mfanyakazi asiende ofisi, kwa kuwa mwanasiasa ofisi yake ni jukwaa la mikutano au mkutano. Ushauri ni kwamba, naiomba Serikali katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu hali hii ingeangaliwa upya.