Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mawaziri walio chini ya ofisi yake kwa utendaji wao uliotukuka. Pia nipongeze hotuba yake nzuri na bora yenye dhamira ya kuifanya nchi hii ijitegemee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kitabu cha hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ukurasa wa 42 ameonesha nia na dhamira ya Serikali ya kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo ya nchi yetu. Ipo dhamira ya Serikali ya kuunganisha mikoa yote kwa kiwango cha lami. Mkoa wa Singida unaungana na Mkoa wa Mbeya kwa njia ya barabara. Barabara hii imejengwa toka Mkoa wa Mbeya, Serikali ilionesha nia ya kuanza kujenga kutokea Mkoa wa Singida kutoka Mkiwa Itigi hadi Moranga kilometa 56.9 na mkandarasi alipatikana ambaye ni SIMOHYDRO.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alipokuwa anafungua barabara ya Manyoni – Chaya kilometa 89 tarehe 25 Julai, 2017 alibaini mchakato wa zabuni ulikuwa na harufu mbaya na akatoa maelekezo yaliyosababisha barabara hii kutokujengwa au kuanza kujengwa hadi hivi leo. Je, ni lini sasa Serikali itaona ni vyema kuwatendea vyema wananchi wa jimbo langu kwa kuanza kuijenga barabara hii.

Naomba sasa mwaka huu basi Serikali ianze ujenzi wa barabara hii ambayo ni muhimu sana katika kuunganisha Mkoa wetu wa Singida na Mkoa wa Mbeya. Barabara hii ndiyo pekee iliyobaki ya kuunganisha mkoa na mkoa ambayo ni ndefu kuliko zote Tanzania kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii tena kuipongeza Serikali na pia nimpongeze kipekee Mheshimiwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa utendaji wake na juhudi nyingi katika ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa na ununuzi wa ndege na hata vivuko katika maziwa yetu.