Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma mapitio ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2017/2018 ambayo sasa tunaelekea kuandaa bajeti mpya unakuta katika mwaka wa fedha wa 2017/2018, Serikali ilikusanya takribani shilingi trilioni 17 na matumizi yalikuwa shilingi trilioni 18, hii ni kwa mujibu wa kitabu hiki. Kama mapato yalikuwa shilingi trilioni 17.9 matumizi yakawa shilingi trilioni 18.7 maana yake ni kwamba nakisi ya bajeti yetu ilikuwa inakaribia shilingi trilioni 1 na hiyo ama ipatikane kutokana na mikopo ama misaada kutoka nje, matokeo yake bajeti imeshindwa kutekelezwa. Ukisoma bajeti yote, mishahara na matumizi mengine ya Serikali karibu fedha zote zilizokusanywa zimetumika katika matumizi ya mishahara na matumizi mengine ya madeni ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali isiyofikia malengo ya makusanyo yake haiwezi kutekeleza bajeti yake kikamilifu. shilingi trilioni 6 ambazo zilitengwa kwa ajili ya maendeleo hizi zote maana yake hazipo katika makusanyo ya Serikali, zenyewe ni lazima zipatikane ama kutokana na mikopo ama kutokana na misaada kutoka nje. Misaada sasa imekuwa shida kutokana na mahusiano yetu kuwa siyo mazuri na nchi wahisani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye bajeti, kwa mfano, uvuvi, makadirio yalikuwa shilingi bilioni 7.1, fedha za ndani shilingi bilioni 3, fedha za nje shilingi bilioni 4, zilizotoka shilingi bilioni 4 maana yake pengine Serikali haikutoa hata shilingi katika uvuvi. Matokeo yake Serikali imeenda ku-deal na wanaoitwa wavuvi haramu, uvuvi watu hawawezi tena. Hatukuweza kutoa mafunzo tumeishia kulipa mishahara, matokeo watu wanalipwa mishahara, wanakaa ofisini wanasoma magazeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye kilimo, makadirio ni shilingi bilioni 98.1, zilizotoka ni shilingi bilioni 41.2 sawasawa na asilimia 42 plus. Sasa kilimo ndiyo uti wa mgongo wa Taifa hili. Kwenye kilimo ndiko kwenye miwa, kwenye sukari; kwenye kilimo ndiko kwenye chakula, Serikali inashindwa kuwekeza kwenye kilimo, tunategemea wahisani, halafu matokeo yake tunasema tumetekeleza bajeti yetu, tunakaa hapa tunajisifu, tunasema mwakani kusiwe na uchaguzi, tunatumia shilingi milioni 800 Dola za Marekani kuagiza chakula nje, karibu shilingi trilioni 1.8.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo...

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kubenea, subiri kidogo. Taarifa Mheshimiwa Ulega.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa Mheshimiwa Kubenea, kwa faida yake na kwa faida ya Waheshimiwa Wabunge wengine kutokana na kauli aliyoisema kuwa Serikali haiwekezi na hivyo kupelekea wataalam katika Wizara kama vile ya Uvuvi, wanakaa wanasoma magazeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe taarifa kuwa katika Wizara ambazo Serikali imetenda vyema, hata kupelekea kuvuka malengo katika utekelezaji wa kazi, ni Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika mwaka wa 2018/2019 ambao sasa tupo katika robo ya mwisho. Idara Kuu ya Mifugo imetengewa kukusanya pesa za maduhuli ya Serikali takriban shlingi bilioni 18. Mpaka hivi sasa tunavyozungumza, tumeshakusanya shilingi bilioni 26. Maana yake ni kwamba tuko zaidi ya asilimia 140. Idara kuu ya Uvuvi ilipangiwa kukusanya shilingi bilioni 16, mpaka sasa hivi tumeshakusanya zaidi ya shilingi bilioni 24. Maana yake tuko zaidi ya asilimia 110. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Mbunge anaposema kuwa watu wamekaa wanasoma magazeti, ni kwa sababu sio mfuatiliaji wa haya mambo. Nampa nafasi afuatilie zaidi ili aweze kuona mchango chanya unaotokana na Idara kubwa hizi mbili kwa mapato ya Taifa letu. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kubenea.

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba unilindie muda wangu. Anaposema maduhuli, maana yake ni kodi, maana yake ni faini. Haya siyo makusanyo yanayotokana na fedha za kodi, ni faini. Ndiyo maana Ziwa Victoria Tanzania inamiliki zaidi ya asilimia 50 ya Ziwa Victoria; Uganda wanamiliki asilimia 33; na Kenya wanamiliki asilimia 6. Tokea Serikalli ya Awamu ya Tano iingie madarakani, viwanda saba vipya vimefunguliwa Uganda na Watanzania, kwa sababu ya urasimu uliopo kwenye Wizara ya Mifugo na Uvuvi; kwa sababu ya kuweka sheria za operesheni hizo za wavuvi. Watu wamekimbia nchi wameenda kuwekeza Uganda kwa sababu ya faini hizo za shilingi bilioni 20 anazodai hapo Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunapozungumza, hii niliyosoma, shilingi bilioni tatu ni ya Wizara yenyewe, kwamba fedha iliyopelekwa ni shilingi bilioni tatu, siyo ya kwangu mimi. Sasa anapozungumza kwamba wamekusanya, kukusanya maduhuli, maduhuli sijui anaelewa maana ya maduhuli? Maduhuli siyo kodi ya kila siku ya Serikali, ni vyanzo vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona niachane naye.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ndiyo uti wa mgongo. Pembejeo zote zinazopatikana kwenye kilimo…

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Agness, taarifa.

T A A R I F A

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampa taarifa mwongeaji, pale aliposema kwamba Tanzania hatuna mahusiano mazuri na nchi wahisani. Labda kama hana kumbukumbu nzuri.

Mheshimiwa Mwenuekiti, majuzi Chancellor Merkel, Rais wa Ujerumani, aliipongeza Tanzania kwa kuwa na mahusiano mazuri na nchi nyingine na kwamba uchumi wetu umekua sana. Pia nampa taarifa kwamba juzi tumefungua Ubalozi mpya…

MWENYEKITI: Imetosha, taarifa ni moja tu bwana.

MHE. AGNESS M. MARWA: …Cuba ambao yeye anapaswa kuji…

MWENYEKITI: Hapana taarifa ni moja tu.

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kubenea, taarifa moja tu ile ya kwanza.

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mimi hiyo taarifa wala sina sababu nayo kuipokea kwa sababu mimi nimepokea taarifa ya Serikali yenyewe, Mheshimiwa Waziri ameeleza ndani ya bajeti kwamba mahusiano yao siyo mazuri na wahisani, kwa hiyo, wahisani hawatoi hela vizuri. Hata hii inathibitisha.

MWENYEKITI: Kwenye ripoti gani hiyo wewe Mheshimiwa?

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi ni…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kubenea, hebu nisaidie na mimi ili record ikae vizuri. Kwenye taarifa ipi?

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mradi wa Mheshimiwa Zitto Kabwe, alikuwa na mradi kule Kigoma, ambao...

MWENYEKITI: Hapana. Mheshimiwa Kubenea, hapa tuna hoja ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, wewe niambie tu katika andiko.

MHE. SAED A. KUBENEA: Nimeiondoa, nichangie. (Makofi)

MWENYEKITI: Haya.

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nimemsikia Mheshimiwa Rais anasema kwamba viwanda vyote ambavyo vimebinafsishwa na Serikali na wale ambao walipewa kazi ya kubinafsisha viwanda hivyo ambao walibinafsishiwa viwanda hivyo, hawakuviendeleza wavirejeshe Serikalini. Mheshimiwa Rais akaomba radhi kwa niaba yake binafsi na kwa niaba ya watangulizi wake kwa mambo ambayo yalifanyika katika nchi katika uuzaji na ubinafsishaji wa mali za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais amesahau jambo moja kubwa sana ambalo limefanyika katika nchi hii. Nyumba za Serikali zilizouzwa Rais hajasema zirejeshwe, tunaomba nyumba zote za Serikali zilizouzwa kiholela na kienyeji, zirejeshwe mikononi mwa Umma. Nyumba hizi waliouziwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)