Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu. Pili, nawashukuru wapiga kura wangu wa Jimbo la Kilwa Kusini kwa kuongea nao kwa muda mfupi baada ya sintofahamu ya chama chetu ya muda mrefu na hatimaye mgogoro umemalizika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamshukuru Jaji kwa kutumia hekima kuumaliza mgogoro kwa njia ya kisayansi. Sasa chama ni kimoja na Wabunge wa CUF ni Wabunge wa CUF hakuna lile swali la CUF gani, sasa hivi CUF ni moja. Kwa hiyo, tunamshukuru sana Jaji aliyehukumu kesi hii. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachangia hotuba ya Waziri Mkuu, ukurasa wa 15 umezungumzia hali ya kisiasa na Mheshimiwa Waziri Mkuu amejisifu kwamba hali ya kisiasa ni nzuri na kulikuwa na chaguzi za marudio na CCM imeshinda kata 230, CHADEMA kata moja, CUF hakuna kitu. Mimi siamini kwamba ushindi huu wa kata 230 na CHADEMA kushinda kata moja kwamba uchaguzi huu ulikuwa huru na wa haki. Siamini kabisa na hali ya kisiasa katika nchi yetu ni mbaya mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa mfano katika Wilaya yangu ya Kilwa tulingombea kata tatu na CCM zote wakashinda. Hata hivyo, Polisi waliojaa katika uchaguzi huo wa kata tatu utasema kuna vita ya Vietnam na Marekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika uchaguzi huo Janjaweed wa CCM waliwateka watu watatu. Tarehe 27 walimteka kijana mmoja anaitwa Abdulrahman Bungara, wakampiga, ni mwanachama wa CUF, wakamnyang’anya saa na hela. Tarehe 29 hao hao watu wa CCM wakampiga kijana mmoja jina lake Shaban Mkongo wakamnyanganya fedha. Tarehe 2 siku ya uchaguzi walimteka Juma Ngondae, wakampiga na wakamfikisha Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa wote tulifungua mafaili ya kesi lakini mpaka leo hajakamatwa mtu hata mmoja. Waliokuwa wanafanya matukio hayo wanajulikana na gari waliyokuwa wakitumia kuwateka watu hao inajulikana na gari hiyo ni ya Mbunge mmoja ambaye yupo humu humu ndani. Tumefungua kesi lakini mpaka leo hawajakamatwa lakini mwenye gari tunamjua ni ya aliyekuwa Mbunge wa CUF sasa hivi yupo CCM, gari yake tunaijuwa ndiyo iliyotumika kuteka watu wote hao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zikaja kata zingine tatu, wagombea wetu wakarudisha fomu na ndiyo niliyowapeleka kurudisha fomu. Siku ya siku wakasema fomu za CUF zote hazikurudishwa na wagombea wa CCM wamepita bila kupigwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unapojisifu wewe Waziri Mkuu kwamba tulipita, upitishaji wenyewe wa kunyang’anya, hakuna siasa safi na uongozi bora katika nchi hii. Tunaamini kabisa kwa Tume hii ya Uchaguzi 2020 tegemeeni kutakuwa na vita kubwa sana kati ya wananchi na watu wa Tume. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Uchaguzi Mdogo ndiyo mnachukua Jeshi zima, mnapeleka Kilwa Kivinje Jeshi zima, Kilwa Kivinje mnaleta Jeshi zima, je, Uchaguzi Mkuu mna Jeshi ninyi la kusambaza Tanzania nzima, jeshi hilo mnalo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nashangaa sana CCM inashindaje? Nyavu za watu mnachoma moto, watu mnawateka, mnawapoteza, korosho zao hamuwalipi vizuri, wakulima mnawauzi, wafanyakazi mishahara hamuwapi, wavuvi…

MWENYEKITI: Wewe na mimi ndiyo nakumalizia hapo hapo, ahsante kwa mchango wako, tunaendelea.

WABUNGE FULANI: Aaaaaa.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Hata bila kengele?

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Sasa ikiwa kwamba…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Selemani, muda wako umeisha. Tunaendelea na Mheshimiwa Kubenea.

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, muda ulikuwa bado.

MWENYEKITI: Hapana, tulia Mheshimiwa. Mheshimiwa Kubenea.