Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. GODBLESS JONATHAN LEMA (MB)

Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. GODBLESS JONATHAN LEMA (MB)

EMANUEL A. MWAKASAKA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE: Mheshimiwa Spika nakushukuru kwa kupewa nafasi ya kuhitimisha hii hoja. Labda kuja jambo moja ambalo amelisema Mheshimiwa. Kuna hili ambalo alikuwa analizungumzia Mheshimiwa Mnyika la kunukuu Ibara ya 63, lakini pia akanukuu kanuni ya 5 na amenukuu kanuni hizi ili kujaribu kutafuta uhalali kwamba ametumia vifungu na kujaribu kutaka kuonesha jamii au hata wananchi kwa ujumla wadhani kwamba ulichokifanya pengine umekiuka Katiba au kifungu chochote cha kanuni, kitu ambacho si kweli.

Mheshimiwa Spika, Kanuni ya 74, kanuni ya 72(1) inakupa mamlaka ya kuangalia amani na utulivu Bungeni, ninaomba kwa ridhaa yako nisome 72(1) inasema:

“Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibu bora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolote la utaratibu utakuwa ni wa mwisho.” Hii ni kanuni ya 72(1) ya kanuni zetu za Kudumu za Bunge.

Kanuni ya 74(1) inasema:

“Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharau mamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikiwa

(a) kwa maneno vitendo, Mbunge huyo anaonesha dharau kwa mamlaka ya Spika; au

(b) Mbunge huyo atafanya kitendo chochote cha makusudi au Mbunge yoyote anayeongoza shughuli hiyo.”

Mheshimiwa Spika, kitu ambacho Mheshimiwa Lema alikifanya hapa. Kwa hiyo, hakuna mahali popote ambapo umekiuka kanuni yoyote.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Lema jana alisema kitu cha ajabu sana, kwamba yeye alichokisema humu Bungeni na kipo kwenye hansard cha kudhalilisha Bunge na kuliita dhaifu ni msimamo wa Kambi ya Upinzani na leo tunaweza kuthibitisha kwa jinsi walivyoweza kutoka wote hapa, kumbe kweli wao msimamo wao ni kulidhalilisha, kulidharau Bunge. Kwa mantiki hiyo, kwa kuwa tayari tumeshamtia hatiani Mheshimiwa Lema kwa kutohudhuria Mikutano mitatu ya Bunge, Waheshimiwa wengi wote wameweza kuunga mkono pia hoja hii.

Mheshimiwa Spika, naliomba Bunge lako Tukufu liweze kupokea taarifa hii ya Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, lakini pia kuridhia azimio la adhabu ya Mheshimiwa Lema ambayo imependekezwa na Kamati ya Haki Kinga na Mamlaka ya Bunge.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Spika, naafiki.