Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. GODBLESS JONATHAN LEMA (MB)

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. GODBLESS JONATHAN LEMA (MB)

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami naomba niweke maneno yangu machache. Katika Bunge hili baada ya kuapishwa huwa tunapewa vitabu vya kanuni, sasa kwa bahati mbaya Wabunge wengi huwa hawavisomi hivi vitabu vya kanuni, wanasoma mistari michache ambayo wao wanaona wameilewa, lakini hawafanyi jitihada za kuelewa kanuni zote zilizoandikwa katika kitabu hiki cha kanuni.

Mheshimiwa Spika, naomba nisome kanuni ya 72, Sehemu ya Sita inasema hivi:

“Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibu bora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolote la utaratibu utakuwa ni wa mwisho.”

Mheshimiwa Spika, hili Bunge ni la kwako, hizi kanuni ndio zinazokulinda tafadhali asikuchezee mtu yeyote kazi unayoifanya ni nzuri sana na Wabunge tunailewa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeomba kuchangia kwa kuwa juzi nilichangia kuhusu Kamati hii ya Madili lakini jana wakati naingia katika viwanja vya Bunge katika lile geti la usalama kwenye kamera pale kwenye sehemu ambayo tunapekuliwa nilikutana na Wabunge wawili Mbunge mmoja anaitwa Haonga na mwingine wa Mbeya simkumbiki jina lake, nitalikumbuka baadaye, walinizodoa sana, walinitukana sana.

Mheshimiwa Spika, nakupa tu taarifa hii, kwa kuwa mimi kijana nikawaambia kuwa wafanye haya mambo wakiwa katika viwanya Bunge, wakithubutu kufanya nje ya viwanja vya Bunge watakuja kuwasimulia ndani nitakachowafanya. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, juzi nilisema kuwa katika hili Bunge tuna viongozi wetu. Sisi wa Chama cha Mapinduzi tuna viongozi wetu usipohudhuria vikao vitatu unaandikiwa barua, uki-misbehave unaitwa kwenye Kamati za Chama, hawa wenzetu viongozi wao wanapokutana, wakimaliza suala la kuchangishana hamna jambo lingine, kuwa mbunge ahudhurie kwenye vikao asihudhurie lwake, inafika kipindi mpaka Mbunge anafukuzwa Ubunge, kiongozi wao hajui. Kiongozi wao mwenyewe ukihesabu katika vikao vinavyozidi 150 kwa mwaka anavyohudhuria hata vikao hata 20 havifiki. Kwa hiyo hawa wenzetu hawana viongozi. Kwa hiyo ifike mahali tubadilishe hizi kanuni Kiongozi wa Kambi Rasmi Bungeni asipohudhuria vikao kadhaa na yeye mwenyewe aenguliwe, wapewe hata CUF. Leo hii tujiulize CUF kwa nini hawasimamishwi, CUF kwa nini hawa-misbehave Bunge? CUF kwa nini hawatoi kauli chafu? Kwa nini ni wao tu? Kuna chama cha ACT humu kwa nini hayawakuti, ni wao tu CHADEMA?

Mheshimiwa Spika, sasa kwa mfano Mheshimiwa Lema wakati anafanya utumbo wake juzi na kiongozi wake wa Kambi ya Upinzani yupo, hafanyi kitu ananyamaza tu na mimi nilisema, kwa hiyo tubadilishe hizi kanuni hawa viongozi wao wawajibike kwa mambo wanayowafanya Wabunge wao. Tabia mbaya za viongozi wa upinzani, kwanza la utoro, hata ukifanya tathmini ya mahudhurio ya Wabunge wa Upinzani ni nusu ya vikao na ni nusu ya Wabunge, Wabunge wengi. Mheshimiwa Lema siku ambayo unamsikia anazungumza ndio kaingia Bungeni, lakini siku zote hayupo. Anakuja humu kwa ajili ya interest zake na ukiona kaingia ujue ana jambo lake binafsi, sio jambo la watu wa Arusha.

Mheshimiwa Spika, ndio maana ulisema kuwa ukiweka masuala yako binafsi katika Bunge hili, lazima utaharibikiwa, sehemu, acha ya huyo, kuna Mbunge mwingine wa ACT anazunguka huko mitandaoni, anasema anawasainisha wananchi ili wakatae maazimio ya Bunge. Siku moja nitakuja kuwaambia, anayofanya ana interest yake binafsi, sio kama ya jamii kama wanavyojua. Siku moja nitawaambia wananchi na wataelewa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo sisi tunasema, Bunge letu linaenda vizuri na ndio maana maendeleo yanapatikana, barabara zinajengwa na miradi mikubwa inafanyika na wageni wanakuja.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naunga mkono hoja ya Kamati.