Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. HALIMA JAMES MDEE (MB)

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. HALIMA JAMES MDEE (MB)

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Hili ni Bunge, katika nchi yoyote Bunge ni kitu kikubwa ambacho kinaheshimika. Ndani ya Bunge ili kuleta balance na kuwa na nidhamu kuna kiongozi wa upande wa Serikali (Chief Whip) na kuna Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani.

Mheshimiwa Naibu Spika, haya yote tunayoazimia inatakiwa twende extra miles. Kwa nini nasema hivyo? Tukiacha Mheshimiwa Halima Mdee, juzi Mheshimiwa Nassari ameenguliwa Ubunge kwa mujibu wa Katiba, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani yupo na hajui nini kinachoendelea. Mheshimiwa Esther Bulaya, Mheshimiwa Sugu na Mheshimiwa Mnyika wamewahi kusimamishwa Ubunge Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani yupo. Imefika wakati wa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani kujitafakari.

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwa Mheshimiwa Halima Mdee. Mheshimiwa Halima Mdee nipo naye kwenye Kamati moja, ndani ya Kamati ana mchango mkubwa na mzuri kweli kweli. Mimi sijui nini kinamkuta akiwa hapa na mimi ni rafiki yangu na amenishauri vitu vingi sana lakini hapa mambo anayoyafanya; amewahi kufanya kosa mara ya kwanza na ya pili ameadhibiwa, hayo mambo tulitakiwa tufanye sisi kwa umri wetu na uchanga katika Bunge lakini anayafanya yeye. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Halima Mdee alishawahi kupewa nafasi mama yake mzazi kumuombea msamaha katika Bunge hili, hakuna Mbunge aliwahi kupewa nafasi hiyo. Sisi tusio na mama tukifanya makosa tunafanyaje? Mwenzetu amefanya makosa mpaka inafika kipindi wazazi wake wanakuja kumwombea msamaha, sasa hii imekuwa mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kwa matukio hayo naunga mkono Maazimio ya Kamati. Ahsante sana. (Makofi)