Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. HALIMA JAMES MDEE (MB)

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. HALIMA JAMES MDEE (MB)

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Sidhani kama naweza nikashawishi Bunge kuondoa adhabu ambayo imeshakuwa proposed na Mwenyekiti wa Kamati. Maneno yafuatayo ndiyo yanamfanya Mheshimiwa Halima apendekezewe adhabu kubwa kwa kiwango hicho. Nnaomba niyanukuu: “Kitendo cha CAG cha kusema kwamba hali siyo nzuri halafu chombo kinachotakiwa kusimamia hali hakifanyi hivyo, ni kitendo cha kijasiri na nina imani kwamba wanaoongoza huo mhimili watakuwa wavumilivu, hawatafikiria kumuita kwenye Kamati ya Maadili kwa sababu tumeitwa dhaifu kwa sababu kweli ni dhaifu. Roho ya mwenendo wa nchi unategemea uimara wa Bunge. Sasa amesema Bunge ni dhaifu ni kweli na mimi kama Mbunge wa vipindi vitatu nathibitisha hilo.” Mimi ni Mbunge wa vipindi viwili nathibitisha Bunge hili ni dhaifu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Lema kwa maneno hayo uliyoyasema na wewe unapelekwa kwenye Kamati ya Maadili na ukae hakuna mchango tena. Kwa sababu tunajadili adhabu kuhusu maneno hayo na wewe unasema unayathibitisha na wewe utaelekea kwenye Kamati ili ukathibitishe vizuri kule. Kwa hiyo, Kamati ya Maadili huyu naye analetwa kwenu kwa utaratibu wa kawaida. (Makofi)

Tunaendelea na Mheshimiwa Goodluck Mlinga.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Naibu Spika, huna...

NAIBU SPIKA: Umeshapewa adhabu Mheshimiwa kwa hiyo wewe…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Lema, naomba ukae, Mheshimiwa Lema naomba ukae.

Tunaendelea na Mheshimiwa Goodluck Mlinga, tutamalizia na Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma.