Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie katika hoja iliyoko mbele yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Profesa Assad kwa kuwa mkweli. Profesa Assad kawa mkweli, kasema ukweli wake, kasimama na ukweli wake na kasimama na anachokiamini katika taaluma yake. Pia nampongeza kwamba hakuisumbua Kamati kwa sababu kasema alichokisema na kasema mbele ya Kamati anachokiamini kwa mujibu wa taaluma yake. Kwa hiyo, mimi nampongeza sana Profesa Assad. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikiliza msomaji hapa wa taarifa sijaona sehemu yoyote ambayo Profesa Assad ana sababu ya kutiwa hatiani. Kama mtu kakiri alichokisema na kasema hicho nimesema na ndivyo taaluma yangu inavyosema, nyie mnamtia hatiani kwa sababu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi sioni sababu ya Profesa Assad kutiwa hatiani kwa hiki alichokisema kwa sababu hajabadilisha neno na wala hajakataa, kasema. Kuona sisi Wabunge kwamba tunaweza au tunajua kila kitu ni kosa. Tukiambiwa dhaifu lazima tukubali, sisi ni wanadamu hatujakamilika lazima tuna madhaifu yetu. Kwa hiyo, tunapokosolewa lazima tukubali kukosolewa. Sasa kama kuna udhaifu na ni wanadamu sisi si Mungu lazima tukubali kuna udhaifu, no one is perfect. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwamba sisi tusikosolewe, hii tutakuwa sasa tumekiuka mipaka. Kwa hiyo, mimi nampongeza sana Profesa Assad na Kamati sijaona kama imetutendea haki kwamba sisi tusikosolewe, sisi ni nani mpaka tusikosolewe? Sisi ni wanadamu kama mwanadamu mwingine yeyote. Awe ni raia wa kawaida, Mbunge, Waziri, Rais kama ni mwanadamu lazima atakosea na huo ndiyo uanadamu, ile kutenda makosa ndiyo uanadamu wenyewe. Kwa hiyo, lazima tukubali kama ni udhaifu basi kweli tunao kwa sababu sisi ni wanadamu, tuangalie sasa udhaifu huu uko wapi na nini tufanye. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama tuna watu kama hawa anaweza akasimama akakwambia hapo umekosea wewe unamhukumu kwa kukwambia hilo wakati umekosea kweli, hatutendi haki. Kuna mifano mingi, tumetunga sheria ngapi humu zimekwenda huko, zimerudi tunazifanyia amendment, je, tuko perfect? Kwa nini kila tunachokifanya kikienda huko kisiende smoothly, kwa nini kirudi tufanyie amendment? Ni kwa sababu sisi ni wanadamu tuna udhaifu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwasilishaji kasema kwamba hakuwasiliana na Spika alipoondoka kwenda huko, kwani yeye aliambiwa akienda huko Marekani ataongea na waandishi wa habari na watamuuliza swali hili? Hakujua!

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Yussuf unachangia ukiwa umeweka mikono mfukoni. Hapa ni Bungeni unajua! Eeh, hapa ni Bungeni na kengele imeshagonga.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, kengele ya kwanza.

NAIBU SPIKA: Kengele ni moja tu Mheshimiwa Yussuf.