Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja hii muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaingia kwenye hoja, naomba nisome andiko katika Amosi 3:3 ambalo linasema: “Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema neno hilo sasa niingie kuchangia hoja hii. Mimi ni Mwanakamati wa Kamati ya Maadili kwa jinsi ambavyo tulimhoji CAG na jinsi ambavyo alionyesha kwa kweli dharau kubwa ya kulidharau Bunge na hakuonyesha kujutia kitendo kile.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini CAG ni jicho la Bunge na Serikali. CAG ni mtu ambaye anaanimika sana. Mimi nilikuwa najiuliza swali moja, hivi jicho linaweza likauambia mwili wewe hufai? Kitendo cha CAG kusema Bunge ni dhaifu ni pamoja na kusema Rais wa nchi hii ni dhaifu kwa sababu Rais ni sehemu ya Bunge, Waziri Mkuu ni sehemu ya Bunge lakini na sisi Wabunge hapa ni sehemu ya Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kitendo alichokionyesha CAG ni cha dharau, kulidhalilisha Bunge na kuidhalilisha Serikali yetu. Kwa hiyo, naungana na hoja ambayo imeletwa mbele yetu kwa kweli hatuwezi kuendelea kufanya naye kazi kwa sababu hakulidhalilisha Bunge peke yake ni pamoja na Mheshimiwa aliyemteua kwa sababu na yeye ni sehemu ya Bunge lakini na Mawaziri wote ni sehemu ya Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme CAG hakuonyesha uzalendo wowote. Tumekuwa tukiona Mataifa mengine haijawahi kutokea kiongozi mkubwa namna hii hata kama kuna upungufu kusimama na kuanza kuidhalilisha Serikali namna hii.

Kwa hiyo, kitendo alichokionyesha CAG kinakiuka hata maadili ya kiapo chake.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ninaunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)