Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Hon. Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI NDUGU PROF. MUSSA ASSAD, MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na umahiri mkubwa wa CAG nafikiri kuna umuhimu wa viongozi kuzingatia kauli zao hasa kulinda uzalendo wa nchi yetu. CAG amekwenda Marekani matokeo yake anaponda Bunge, anasema Bunge dhaifu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mimi namwambia CAG Bunge siyo dhaifu, Spika wetu siyo dhaifu, kuna mengi sana ya kuongelea mazuri kuhusu Bunge hili. Nilitegemea msomi kama CAG atayaongelea hayo matokeo yake amesema Bunge dhaifu kitu ambacho ni kinyume kabisa ni kwamba CAG ameongea uongo Bunge siyo dhaifu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, CAG pamoja na yote hayo tulisema labda aliteleza. Ameitwa na Kamati ya Bunge bado ameendelea kuonyesha jeuri akiendelea kusema ataendelea kuitumia kauli hii. Sasa sisi hatuko tayari kuendelea kuitwa dhaifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, CAG amekuwa akifanya kazi na Kamati ya PAC na LAAC, sidhani kama kuna chochote alifikisha huko kikashindikana matokeo yake ameenda kuongea nje ya nchi, ameshindwa hata kulinda Taifa lake amekwenda kutusema kwenye mataifa ya nje ambapo dunia nzima wamesikia kumbe Bunge dhaifu. Kwa hiyo, kauli hiyo tunaikataa kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile CAG alikuwa na muda alivyoitwa na Kamati kusema basi hata asamehewe matokeo yake ameendelea kurudia kauli hiyo. Amesema ni lugha ya kiuhasibu, mimi sijui kama wahasibu wana lugha ya udhaifu, ametudhalilisha na amelidhalilisha Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, naungana kabisa na Kamati hatuko tayari kufanya kazi na CAG ambaye ameshatudharau na kutuita sisi dhaifu. Naungana na hoja ya Kamati. (Makofi)